Tafuta/Search This Blog

Thursday, September 26, 2013

AUTO TREND WITH SAUDI YOUTH.








Two current automobile trends with youths in Saudi Arabi right now include a dangerous stunt known as “sidewall skiing” (driving on two wheels) and "stoning," in which cars are raised atop stacked piles of rocks and bricks.

Picha za Yahoo News

Rais Kagame aongeza sauti yake kwa wakosoaji wa ICC

Rais Paul Kagame wa Rwanda, leo ameongeza zauti yake kwa zile za viongozi wa Afrika ambao wameishutumu mahakama ya kimataifa ya uhalifu, ICC, kwa kuwalenga tu viongozi wa Afrika.
Katika hotuba yake kwenye mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Jumanne mchana, Bwana Kagame amesema Waafrika waliunga mkono muafaka wa kimataifa wa kuhakikisha wahalifu wanawajibishwa, na kubuniwa kwa mfumo wa kimataifa wa sheria wa kukabiliana na uhalifu kama huo, wakiamini kuwa mfumo kama huo ungeendeleza amani na usalama ndani na baina ya nchi, na kuendeleza usawa wa uhuru wa nchi zote. Badala yake, Bwana Kagame amesema mahakama ya ICC imekiuka malengo hayo.
ICC imeonyesha upendeleo ulio dhahiri dhidi ya Waafrika, badala ya kuendeleza haki na amani. Imelegeza juhudi za maridhiano, na kutumiwa kuwadhalilisha Waafrika na viongozi wao, pamoja na kuhudumia haja za kisiasa za wenye nguvu. Hakuna mahali ambako dosari ya ICC imeonekana zaidi kuliko katika kesi inayoendelea ya viongozi wa Kenya. Watu wa Kenya wameonyesha hamu ya kuponya vidonda vya zamani, kuridhiana na kwenda mbele. Ndio maana waliwachagua viongozi wao wa sasa wanaojibu mashtaka.
Rais Kagame amesema juhudi za maridhiano ya kijamii na kuendelea zinatakiwa ziungwe mkono, pamoja na juhudi za taasisi za kitaifa kukabiliana na uhalifu, badala ya kudhoofisha juhudi za kuziimarisha taasisi hizo. Amelitaka Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na Baraza la Usalama kulizingatia suala hilo na mengine yanayohusiana na sheria za kimataifa, ambayo tayari yamewasilishwa kwao, ili kudumisha haki, usawa wa kimataifa, kuunga mkono juhudi za maridhiano na kuheshimu utu wa Waafrika.

Habari kwa hisani ya Radio.un.org/sw  

Monday, September 23, 2013

Zaidi ya watu 60 wauawa kwenye shambulizi la kigaidi nchini Kenya


Takriban watu 62 wameripotiwa kuuawa na wengine zaidi ya 150 wakijeruhiwa baada ya watu waliojihami wanaokisiwa kuwa wanamgambo wa kundi la Al shabaab kushambulia jumba moja lenye maduka mengi kwenye mji mkuu waKenyaNairobi. Zaidi ya watu 1000 waliokolewa kutoka kwenye jumba hilo la Westgate ambapo pia hadi sasa watu kadha wanakisiwa kushikiliwa na magaidi hao. Jason nyakundi na taarifa zaidi.
 (RIPOTI YA JASON)
Kulingana na Shirika la msalaba mwekundu nchiniKenyani kuwa hadi sasa watu 62 wamethibitishwa kuuwa wengine zaidi ya 150 kujeruhiwa  huku watu 69 hawajulikani waliko kufuatia shambulizihilola kigaidi ambalo limelitikiza taifa laKenyana kuushangaza ulimwengu kwa ujumla. Hawa ni baadhi ya wananchi waliokuwa kwenye jumbahiloambao walifanikiwa kukimbia na haya ni yale walioyashuhudia
 (SAUTI ZA WANANCHI)
Magaidi hao wanaokisiwwa kuwa wangambo la kundi la Al shabaaab kutokaSomaliawalilivamia jumba la Westgate mwendo wa saa tano asubuhi siku ya Jumamosi ambapo walianza kuwafyatulia watu  waliokuwa kwenye shughuli zao risai kiholela . Jumbahilo lina zaidi aya maduka 80 na hutembelwa sanana watu walio na uwezo wa kifedha. Masaa machache baadaye rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ambaye pia alimpoteza mpwa wake wakati wa uvamizi huo alilihutubia taifa akililaani shambulizi hilo.
 (SAUTI YA KENYATTA)
Jumba hilo kwa sasa limezingirwa vikosi vya jeshi la Kenya wanaojaribu kuwaokoa watu ambao bado wanakisiwa kushikiliwa mateka na magaidi hao huku milio ya risasi ikisikika mara kwa mara kutoka kwa jumbahilona moshi mweusi nao mara nyingine ukionekana kutoka kwenye paa la jumbahilo.
Wakati hayo yakijiri mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ICC imemruhusu makamu wa raias wa Kenya William Ruto ambaye amekuwa mjini Hague tangu juma lililopita akihudhuria kusikilizwa kwa kesi inayomkabili kuhusiana na uhalifu wa kivita kurudi nyumbani kwa kipindi ya juma moja baada ya yeye kutoa ombi la kutaka kurudi nyumbani kushughulikia hali iliyo sasa nchini Kenya baada ya kutokea kwa shambulizi la kigaidi.

kwa hisani ya : Radio.un.org/sw  

KENYA, We are praying for you!!!


Wapendwa wetu waKenya,

Tunafahamu ugumu wa hali mnayopitia wakati huu. Tunalia pamoja nanyi na kwa kweli kitu pekee tunaweza kukifanya wakati huu ni KUWAOMBEA. Tunawakumbuka sana katika maombi ili wakati huu upite na Mungu awatie nguvu za kuvumilia na kuwapunguzia ugumu na uzito wa majonzi haya.

Tunafahamu kwamba matendo kama haya yanadhihirisha UWOGA wa maadui zetu, na tunajua adui huyu mtamshinda kwa UMOJA wenu. Kwa hiyo pigeni moyo konde na umoja wenu na utaifa wenu uongezeke sana sasa maana wakati kama huu mnahitajiana zaidi.

Mungu awe nanyi daima!!
We are praying for you!

SBP.

Magazeti ya leo Jumatatu tar 23 Sept 2013












Wednesday, September 18, 2013

UHUSIANO WA KIBALOZIKATI YA NCHI YA CHINA NA NCHI YA CCM.....

CCM & China friendship

Nissan NAVARA INAUZWA!

With rain Cover


Without rain cover

Without rain cover

Nissan Navara, 2.5 Diesel, 2004.
This Car is already in Mwanza, Tanzania.
Serious buyers only;

Call Fred: 0713740770/0785740770

Or call any numbers of the owners of this blog.

Friday, September 6, 2013

Tanzania VS Rwanda.... SULUHU HII IWE YA KUDUMU.

Maneno ya Rais wetu Mh, Jakaya Mrisho Kikwete kuhusu Rwanda
 Alisema....
“Isitoshe, ushauri ule niliutoa pia kwa serikali za DRC, na Uganda. Katika mkutano ule Rais Museveni wa Uganda aliunga mkono kauli yangu.
Rais Kagame hakusema chochote pale mkutanoni. Baada ya kurudi nyumbani ndipo tukaanza kusikia maneno tuliyosikia na tunayoendelea kusikia.
“Kwa upande wangu sijasema lolote kuhusu Rwanda pamoja na maneno mengi ya matusi na kejeli yanayotoka kwenye vinywa vya viongozi wa Rwanda dhidi yangu. “Si kwamba siambiwi yanayosemwa au sijui kusema au sina la kusema, la hasha, sijafanya hivyo kwa sababu sioni faida yake,” 

Sitamani Kagame afanye haya tenaaaaaaaaaaaa. yaani baada ya kikao aende kuongea chochote huko kwao.

Thursday, September 5, 2013

BWANA KAMAU MKENYA ANAYEFANYA KAZI YA KUTENGENEZA NYAMA CHOMA HUKO MAREKANI

Naamini unaweza kutokwa na Mate kwa sababu hii.......





HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI (MNH) WAPATIWA MSAADA WA MAGODORO 50 KUTOKA NEEMA WOMENS POWER GROUP CHA JIJINI DAR ES SALAAM. MEYA WA ILALA JERRY SILAA ALIKUA MGENI RASMI.

Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ta Taifa Muhimbili Sr. Agnes Mtawa akitoa hotuba fupi pembeni ya mgeni rasmi Mstahiki Meya wa manispaa ya Ilala Ndg Jerry Silaa katika tafrija fupi ya kupokea magodoro 50 kutoka katika kikundi cha akina mama cha NEEMA WOMENS POWER katika ukumbi wa mikutano wa Muhimbili (Board Room)

Katibu wa kikundi Mama Dedes akisoma hotuba ya kikundi katika hafla ya kukabidhi msaada wa magodoro 50 katika hospitali ya Taifa Muhimbili. Alieleza mpango wa kikundi ni kutoa magodoro 3000 kusaidia wanawakw na watoto wanaolazwa katika hospitali za mkoa wa Dar es salaam. Aliwahimiza woote waliopata kadi za kuchangia wanakumbushwa kutoa michango yao ili kutimiza ahadi ya magodoro 3000 waliyoitoa. 


His Worship the Mayor Jerry Silaa, Akikabidhi Magodoro 50 kwa Kaimu mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kama msaada uliotolewa na kikundi cha wanawake kiitwacho NEEMA WOMENS POWER GROUP
Picha kwa hisani ya Blog ya Michuzi

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS

DSC 0020 2b75e
DSC 0021 88774
DSC 0022 ba93e
DSC 0023 35131
DSC 0024 491a2

DSC 0025 64822
DSC 0026 99213
DSC 0027 46f3c
DSC 0028 6ea69
DSC 0029 7e185