Tafuta/Search This Blog

Monday, October 28, 2013

KONGAMANO KUBWA LA UAMSHO NA MAOMBEZI



Kanisa la T.A.G Kigogo Mburahati Limekuandalia Kongamano kubwa la UAMSHO NA MAOMBEZI.

Tarehe: 28 Oct. hadi 3 Nov 2013

Muda: Saa 10:00 – 12:00 Jioni

Wahudumu: Askofu Laurence Kameta, Mch. Sir Gilbert, Mwinjilisti Crispin Madembwe pamoja na
Mch. Sabinus Mbogo.

Kwaya zitakazo hudumu ni Kinondoni Revival, Peace Maker Ilala na Wenyeji T.A.G Kigogo kwaya waimbaji binafsi watakao hudumu ni Lyanga George na Sara Shira.

Wenye shida mbalimbali kama Matatizo ya ndoa, Magonjwa, waliofungwa na Mapepo na matatizo mengine yote YESU MTENDA MIUJIZA ATAYASHUGHULIKIA! NJOO UKUTANE NA MUNGU!

Kanisa liko karibu na Kituo cha Mburahati msikitini mita chache sana kuelekea barabara ya barafu.

Kwa mawasiliano 0754 995 590 au 0712 554 528

Hatimaye Papaa Samuel Sasali a.k.a the Blogger ameoa!

Jana, tarehe 26 Oktobe ilikuwa siku ya kihistoria sana katika ngome ya mabachela nchini Tanzania baada ya bachela Nguli kujiondoa rasmi kwenye hilo kundi na kujiunga kwenye klabu ya waliooa! Sisi SBP tunawapongeza sana Sam na Mirembe kwa hatua hii na tunawatakia maisha mema ya ndoa

Smiles all over! Samuel na mke wake Mirembe.
Mambo haya yasingekosekana asilani!!


Ukweliii1



Hii picha muhimu sana! Nahisi Papaa alikuwa anamkabidhi rafiki yake Prosper Kijiti na kuweka msisitizo!

Mr&Mrs Sasali wakisindikizwa na Mr&Mrs Mndeme.

Picha zote zimetolewa Facebook page ya MC LUVANDA

Sunday, October 27, 2013

Sikiliza kuhusu daktari aliyejitolea maisha kuokoa wahanga wa ubakaji!

Denis Mukwege, daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake kwa zaidi ya takribani miaka 15 amejitolea maisha yake kuokoa wahanga wa ubakaji huko mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC. Akihudumia kwenye hospitali ya Panzi huko Bukavu, hospitali aliyoianzisha mwaka 1993, Dkt. Mukwege na wenzake wametoa usaidizi wa kitabibu kwa maelfu ya wanawake waliokumbwa na wanaoendelea kukumbwa na madhila ya ubakaji. Katika makala hii, Joseph Msami alipata fursa kuzungumza na Dokta Mukwege ambaye alifika makao makuu ya Umoja wa Mataifa kwa mazungumzo na Katibu Mkuu Ban Ki-Moon. Katika mazunguzo na Msami, Dokta Mukwege walijadili mengi ikiwemo alivyonusurika kuuawa mwaka mmoja uliopita. 


Monday, October 21, 2013

MILIKI KIWANJA CHAKO POPOTE TANZANIA. KWA WAKAZI WA DAR ES SALAAM VIWANJA MAENEO YA KIGAMBONI, CHANIKA NK

WALE WENYE MAWAZO YA KUJENGA HAPA TANZANIA NA HASA DAR ES SALAAM MSITIE SHAKA TENA, SASA UNAWEZA KUPATA ENEO ZURI LA KUJENGA KWA BEI NAFUU NA KWA UHAKIKA. BEI NZURI YA UNAYOWEZA KUIMUDU HATA MTU WA KAWAIDA. TAFADHALI WASILIANA NA Eneza KWA SIMU HII AKUPE JINSI YA KUMILIKU KIWANJA KWA NAMBA HII.... 0718817706. PIA TAASISI NA MAKAMPUNI WANAOTAKA VIWANJA KWAAJILI YA WAFANYAKAZI. TUWASILIANE TU. 

UTAPATA ENEO LILILOPIMWA USIBUGHUDHIWE NA MTU YEYOTE. MAENEO NI MAKUBWA NA MSAADA WA KUPATA RIGHT OF OCCUPANCY UTATOLEWA KWA WATEJA WETU.

TUNA HAKIKISHA VIPIMO

Friday, October 18, 2013

JIWE KUU - Mwanza.

What a wonderful scene!! I have never seen a rock as big as this! 
Huu mjiwe ni balaa


Eneo la Mihama linaonekana kwa chini.


JIwe kuu!



Mr &Mrs Lwendo above the JIwe kuu.

Umeshawahi kusikia kuhusu Jiwe kuu?? Jiwe kuu ni mwamba mkubwa sana uliopo maeneo ya Bwiru Mwanza. Hili jiwe ni kubwa sana limetapakaa katika eneo kubwa lipo juu sana. Leo nilipata nafasi ya kutembelea huko na kuliona jiwe hili maarufu. Nadhani hii ni sababu nyingine ya hili jiji kuitwa Jiji la miamba. Kama serikali kupitia wizara ya utalii wangetumia fursa, hii nieneo jingine la ukweli sana. Shukrani Kwa GLTI.

Tuesday, October 15, 2013

PROGRAM MAALUM YA REDI YA UM LEO - 15 OCTOBER 2013



Nawatakia kila la kheri kumbukeni mnaweza kupata habari nyingine kupitia  Radio.un.org/sw 

Mwalimu Nyerere miaka 14 baada ya kifo chake, fikra zake zazidi kuchanua

Julius Nyerere, Jabali wa Afrika- Mitizamo toka Arusha hadi Obama, kitabu kilichoandikwa kwa pamoja na Profesa Ali Mazrui na Profesa Linda Mhando. Je nini hasa lengo la kuandika kitabu hiki? Flora Nducha na Assumpta Massoi wa Radio ya Umoja wa Mataifa walipata fursa ya kuzungumza na Profesa Mazrui ambaye alikuwepo katika siku maalum ya kumuenzi Mwalimu Nyerere,mjini New York. Kwanza Profesa Mazrui anazungumzia kilichomtia hamasa