Tafuta/Search This Blog

Friday, November 1, 2013

Kanisa la Mt. Cecilia BUJORA

Najua umewahi kuona makanisa mengi hapa africa ambayo mara zote yamekuwa yakijifananisha na tamaduni za ulaya kutokana na historia ya kanisa ilivyo. Makanisa yote yamekuwa yakijengwa kufananishwa na jinsi makanisa ya KIZUNGU yalivyo na kuitwa majina ya huko yalipoanzia na pia kuwaonesha Yesu na mitume wake kama wazungu n.k

Sasa, kuna kanisa lipo Bujora Mwanza. Hili ni la kipekee! Lilijengwa na mzungu lakini kini limejengwa kwa kufuata tamaduni za kisukuma. Kuanzia jengo na vitu vilivyomo ndani na hata sanamu ndani ni za sura za kiAfrica pamoja na Yesu mwafrica. Inapendeza sana jinsi ambavyo jamii hii ya wasukuma ilivyofikiwa na hawa wamishionari. Hebu jionee mwenyewe hizi picha za kanisa hilo.

Hili ndio jengo la kanisa, na hivi ndivyo wasukuma walivyojenga nyumba zao.

Yesu wa kisukuma!



Madhabahu ambayo imefananishwa na pembe ya ng'ombe. Pembe ilitumuka na wasukuma kuwaita kwenye vikao.


ndani.

Sanamu ya bikira Maria wa kisukuma.angalia hata nywele zimesukwa mtindo wa "twende kilioni"

Viti vya watumishi. Hivi ndio viti vya asili vya wasukuma. Pembeni ni mtungi wa maji kwa ajili ya kubatizia.

Viti vya viongozi. Angalia jinsi rangi zilivyopamba ukuta!


Kinanda cha kwaya.
Kaka Godlove ndani ya kanisa.

Unaweza ukatembelea kanisa hili ambalo lipo Bujora Sukuma Museum, Magu mkoani Mwanza.