Tovuti rafiki

Nani ni Nani!

This is a production house where you will meet talented young men producing Video, Audio and graphic designing!
Media house hii ina wataalamu wafuatao:
Enson Msuya-Video and imagery specialist, marketing. Joshua Lwendo (TangiJ)-Audio and floor Management; Godlove Lwendo-Graphic Designer.

You can contact us by these numbers, 0784 494906, 0756025428 and 0784 992221.

We will be more than ready to serve you for any of the service you will need from us as we have described them thereup.

................................................................................

Monday, February 13, 2012

Monday, January 30, 2012

KVCC HARVEST SUNDAY - DAR TRIP

Jumapili ya tarehe 29 January 2012 ilikuwa ni siku ya mavuno kwa kanisa la Kirumba Valley Christian center hapa Mwanza. Ushirika uligawanywa katika makundi mawili, kundi moja likaenda Dar es Salaam na kundi jingine liliingia kwenye mitaa ya Mwanza kwa ajili ya kufanya ushuhudiaji kwa watu wote. Hii ni katika kutimiza agizo kuu la Bwana wetu Yesu Kristo.

Zifuatazo ni picha za kundi lililokwenda Dar:

Mchungaji Geofrey akiwasindikiza watumishi waliokuwa wamejipanga kuingia kwenye chumba cha kusubiria safari, uwanja wa ndege wa Mwanza.

Ndani ya chumba cha kusubiria kulikuwa na wainjilisti 116 wakisubiri muda wa safari.

Dada Rehema, dada Eliza na Pastor Tina.



Prophetess Fay akiwa na Kaka Isaya.


Ndege iliyobeba wainjilisti ikiwa tayari kabisa kwa safari.


Kaka Allan ndani ya cabin.


Dada Matilda.


Kaka Gee.


Ndani ya Cabin. Watu wakiwa na moto wa kuipeleka injili.



Kaka Gee akiwa na Pastor Tina ndani ya bussiness class.
Ndani ya Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam.


Kundi la kwanya likiwa kwenye basi tayari kwa safari ya kwenda Dar Es Salaam Calvary Temple kufanya huduma.


Kikundi cha sifa cha Dar Es Salaam Calvary Temple Kikihudumia kwenye ibada ya sifa.


Kundi la kutoka Mwanza katika viwanja vya kanisa la DCT.


Kaka Moses Dede akitwangwa Keyboard.


Mama Misana a.k.a Nabii mke akiserebuka ndani ya Bwana.


Mchungaji mwenyeji, Ron Swai akisikiliza kwa makini.


Kikundi cha kusifu na kuabudu kutoka KVCC Mwanza katika Ibada.


washirika wote wa KVCC waliokuwa katika ibada hiyo ya DCT wakitambulishwa kwa wenyeji.


Wainjilisti wakisubiri kugawa karatasi zenye neno la Mungu kwa wakazi wa Tabata.



Mchungaji Vitalis katika mitaa ya Tabata.


Kaka Gee akipozi na wanafamilia wa Lugwisha. Wa kwanza ni dada mkubwa wa familia anayefuata ni mmoja kati ya wakaka na wa mwisho ni mke wa mchungaji Geofrey, pastor Tina.


kazi ya kugawa karatasi za maneno ya Mungu iliwagusa hata waliopita na magari.


Ushuhudiaji mitaani.


Baada ya kazi ni safari ya kurudi nyumbani, Mwanza. Hapa ni ndani ya departure lounge ya JNIA.



Kaka Gee, Hans, Daniel na ndugu King'unza kabla ya kuondoka.


Utukufu unabaki kwa YESU!!

Friday, December 30, 2011

Christmas Celebration at KVCC 2011.

Some shots from the christmas service at Kirumba Valley Christian Center Mwanza.


Kaka Gee leading the song Feliz Navidad!



Dada Deborah praising the king.

Mama Gratian doing her thing!

Kaka Allan doing the praise while kaka Isaya Mwakatobe and kaka Gee are doing the African moves.




*********************************************************************


Familia ya kaka Gee, Inawatakia heri na fanaka katika kuingia mwaka mpya wa 2012!

Friday, December 16, 2011

African Music




Kati ya vitu ambavyo Mungu aliwakirimia waAfrica ni kipaji cha muziki. Watu katika mazingira magumu waliyomo lakini bado wanasauti nzuri sana za kuburudisha unapozisikia. wakati leo mataifa yaliyoendelea yanalia hali mbaya ya uchumi, sisi tumezaliwa katika hali mbaya ya uchumi lakini bado tuna kitu cha kuimba na kufurahi.

Msikilize Lokua Kanza na sauti tamu sana. Ni mmoja kati ya wanamuziki wa Africa ambao kila anachoimba ninaweza kusikiliza!

Mungu Ibariki Africa.

Monday, November 21, 2011

Kumbikumbi!

Msimu wa mvua huwa na neema hizi pia. Jirani yangu aliwakamata hawa chakula wengi akaniletea na mimi. Nilisahau kuwapiga picha hadi walipokuwa mekaribia kabisa kuisha nikaona tufaidi pamoja na wewe mdau. Haya karibu japo mmoja wa kuonja hata kwa macho tu...

Thursday, November 17, 2011

EKA CLIFF BUILDING, MWANZA

Mjengo huu upo mitaa is Isamilo, Balewa na hapa picha ilipigwa kutoka kwenye usawa wa Bismarck rocks.
Karibuni Mwanza.

Gratian, mwanamuziki mchanga....

Wednesday, November 16, 2011

Tunapenda sana KUDHAMINIWA!

Nilipokuwa naperuzi kwenye blogu ya blogger mkongwe wa hapa nchini kwetu leo nimekutana na habari ya ajabu sana kwamba kampuni ya bia Tanzania (TBL) kupitia kwenye kinywaji chake cha Grand Malt IMEDHAMINI graduu ya Mkwawa university Iringa!!! What a news!!

Hii ni ajabu sana kwa kweli! Kwani Mkwawa inamilikiwa na nani?? Na hivi inaingia akilini kwa mtu kwamba chuo kimeshindwa kufanya graduu hadi kipate udhamini?? na je kwani uongozi wa chuo ulikuwa unajua kwamba kuna siku wanafunzi watahitimu??? Nimejiuliza mengi sana na kwa kweli nimeudhika!!!

Tunapenda udhamini sana waTanzania,
Tunadhaminiwa net za kujikinga na Malaria
Tunadhaminiwa matangazo ya kufunga seat belt kwa ajili ya usalama wetu wenyewe...
Tunadhaminiwa matangazo kuhusu mahusiano kwenye ndoa zetu...
Tunadhaminiwa...
Tunadhaminiwa...

Sitashangaa siku hotuba ya rais ikidhaminiwa na USAID au siku kesi ya mahakama ya mwanzo itadhaminiwa na VODACOM!!!

Habari hii inapatikana hapa

Tuesday, November 15, 2011

Tanzania is still so beautiful!!

As i was travelling from Dar es salaam to Mwanza through Morogoro,Dodoma,Singida and Shinyanga i just felt like thanking God for this beautiful country. It is beautiful for sure, we are blessed...
God's arranged rocks near Mwanza.



Sukuma's traditional house. The land is so fertile.

Giant rock at Singida region.


Manyoni - Singida road.

Usimwambie mtu...

Hili kitu bado lipo barabarani. Nililikuta Singida last week.