Tafuta/Search This Blog

Thursday, April 6, 2017

Another new friend!



I just found this cat on the side of the road and it followed me home. I really dont understand...is tis s blessing? Should i call City council for these friends shifting to my house??

Bu this new friend is very cute!!! He is actually matching my carpet.

Im speechless!

Dar Es Salaam kwa ufupi.

Julias Nyerere International Airport.

Julias Nyerere International Airport.

Samaki wa baharini!

Samaki watamu sana

Ujumbe maridhawa kutoka kwenye daladala la Tandika

Daraja la Kigamboni. Hap Kama unaendesha gari jitahidi uendeshe speed chini ya 30Kph. Wamejibanza jamaa humu wanakupiga picha



Dar Es Salaam CBD

Dar Es Salaam CBD

Dar Es Salaam CBD


Thursday, March 16, 2017

FC BARCELONA NA GLENN CUNNINGHAM WANATHIBITISHA KUWA TANZANIA YA VIWANDA INAWEZAKANA



Nilipenda kukimbia tokea nikiwa mvulana. Ilikuwa ni kukimbia maili moja (sawa na kilomita 1.8). Glen alikuwa mvulana na hadithi yake ni ya kweli na kusisimua yenye mkasa unaotupa funzo la kuwa ukiwa na nguvu ya dhamira na kufanyia kazi kile unachoamini hakuna lisilowezekana chini ya jua.
Kwa kifupi hii ni hadithi ya Glenn Cunningham alezaliwa August 4, 1909 huko Kansas nchini Marekani.
Akiwa shule msingi na umri wa miaka 8, siku moja Glenn aliungua moto kufuatia mlipuko mkubwa darasani ulisababishwa na galoni la mafuta ya Petroli. Nyakati hizo kulikuwa baridi kali na kila siku wanafunzi walikuwa na jukumu la kuwasha jiko kwa kutumia mafuta ya taa ili kupasha chumba cha darasa joto. Siku moja, mtu asiefahamika aliweka petroli kwenye galoni badala ya mafuta ya taa. Glenn bila kujua aliwasha moto kama kawaida na kupatwa na mlipuko uliounguza mwili mzima na miguu yake kupoteza hisia kabisa kufuatia kufa kwa mifumo ya ufahamu.
Ushauri wa madaktari ni kuwa akatwe miguu kwani asingeweza kutembea kabisa maishani mwake. Mama wa Glenn aliekuwa anaitwa Rosa alikataa ushauri huo wa kumkata mwanae miguu ulitolewa na daktari. Glenn alikaa hospitali kwenye hali ya kutojitambua (in coma situation) na baada ya siku nyingi fahamu zilirudi na taratibu hisia za ufahamu zikaweza kuwa hai tena.
Baadae Glenn alipata ruhusa ya kwenda nyumban. Akiwa nyumbani alikuwa anawekwa juani na wazazi kwenye kiti cha magurudumu (wheel chair) kama mtu mwenye ulemavu. Kuifanya hadithi hii kuwa fupi kuna siku Glenn aliweza kutembea. Alipofanikiwa kutembea japo kwa kuanguka anguka, aliamini kuna siku anaweza kukimbia. Glenn alikuwa anatafakari na kukiri kitabu cha Isaya 40:31 “Lakini wote wanaomtumainia Mwenyezi-Mungu,watapata nguvu mpya.Wataruka juu kwa mabawa kama tai; watakimbia bila kuchoka;watatembea bila kuchoka."
Miaka kadhaa baadae Glenn aliweka rekodi kadhaa za dunia katika mchezo wa riadha. Ntaziweka rekodi chache hapa chini kwa ajili ya kumbukumbu.
Alimaliza mbio za riadha za Olimpiki ya majira ya joto mwaka 1932 na 1936. Akiwa njiani kurejea kutoka kwenye Olimpiki ya nchini Ujerumani, alipigiwa kura kama mtu maarufu kabisa huko Marekani na wana riadha wenzake wa Olympiki.
Mwaka 1933 Glenn alishinda medali ya Sullivan kwa mafanikio yake katika mbio za kati.
Mwaka 1932 kwenye Olimpiki alikuwa mtu wa 4 katika mbio za mita1500
Mwaka 1936 katika Olimpiki zilizofanyika huko Berlin Ujerumani, Glenn alishinda Medali ya fedha katika riadha, umbali wa mita 1500
Mwaka 1934, Glenn aliweka rekodi ya dunia kwa kukimbia maili moja kwa muda wa 4:06.8. Rekodi hii ilichukua miaka 3 kuvunjwa.
Mwaka 1936, Glenn aliweka rekodi ya dunia yam bio za mita 800.
Kwa kifupi Glenn aliweka rekidi nyingi sana. Tukumbuke, hakutarajiwa kutembea kwa vipimo vya kidaktari kutokana na hali aliyokuwa nayo kufuatia kuunguzwa vibaya na moto. Glenn alistaafu riadha mwaka 1940 akiwa na miaka 31.

Hadithi ya Glenn imenikumbusha mechi ya fainali ya mpira wa miguu kati ya Liverpool na AC Milan ya wakali wa wakati huo kama Andrey Shevchenko, Paolo Maldini, Kaka na Hernan Crespo na wengine wengi. Mpaka dakika 45 zinaisha vijana wa Anifield walikuwa nyuma kwa bao 3-0. Kipindi cha pili, Liverpool chini ya nahodha Steve Gerald walirudisha magoli 3 na kuingia katika changamoto za mikuwaju ya penati. Kwa wapenzi wa soka mnakumbuka, Liverpool chini ya kocha Raphael Benitez, walichukua kombe la klabu bingwa Ulaya 2005 kufuatia kuwashinda AC Milan kwa mikwaju ya penati.
Usiku wa jana kuamkia leo kati ya saa 4.45 usiku na kuendelea FC Barcelona ikiwa chini ya Luis Enrique imeleta historia ya kupindua goli 4-0 za mechi ya kwanza kwa kuibamiza PSG kutoka Ufarasa kwa bao 6-1. Kufuatia ushindi huo, naomba kunukuu maneno machache kutoka kwa wanakabumbu kutoka Calanonia.
Gerard Piqué alisama haya baada ya mchezo… “Tumeona matokeo mengi yakibadlishwa katika soka, ila si kama ushindi huu” akimaanisha kupidua magoli 4-0. Na kufunga mabao 6-1 ndani ya dakika 90. Pique aliendelea kusema….”Yeyote asie-amini, anatakiwa aende na aje tena”
Mtu mwingine ni nahodha wa FC Barcelona kiungo mchezeshaji, Andrés Iniesta, ambae alisema hivi…“Tumeshuhudia kitendo cha kihistoria” Iniesta alihitimisha kwa kusema “Hatukukoma kuamini – kiuhalisia ilikuwa haiwezekani isipokuwa imetendeka” (We never stopped believing — it was virtually impossible but it happened.)
Mpira wa jana kati ya FC Barcelona na PSG una mafundisho makubwa kwetu wanadamu, hususan sisi Watanzania. Tunawajibika kuamini na kutoacha kuamini kwa jambo jema tunalolipigania haijalishi uhalisia wa matokeo ya kushindwa huko nyuma ukoje.

Kwa akili tulizo nazo na tukiamua kuweka juhudi kubwa kuleta msukumo kwenye ujenzi wa Tanzania ya Viwanda hususani lenye nia njema kwa kutengeneza bidhaa zenye uhitaji katika soko. Tunaweza  kubadili maisha yetu  kiuchumi na kuwa sehemu ya kujenga daraja la kada la uchumi wa kati Tanzania
Rasilimali zipo, fursa zipo. Cha msingi tunatakiwa kuweka msukumo na jitihada kubwa ili kupata matokeo tunayotarajia.
Mkusanyiko wa jitihada (concentrated efforts) na imani ya kufanya kile unachokusudia bila kukata tamaa, kunaweza kubadili matokeo na historia ya maisha. Ni kweli Rais Magufuli ana muda wa miezi karibu 17 kati ya miezi 60 ya utawala wa awamu yake ya kwanza. Na matokeo yataonekana kwa wale watakao amua kuwa sehemu ya mchezo kubali matokeo na si kulalamika au kuwa watazamaji.
FC Barcelona wamevuka kwenda robo fainali ndani ya dakika 90. Tumbuke, goli 3 zimefungwa kuanzia dakika ya 87 ukijumlisha na muda wa ziada (extra time).
Watanzania, tuna nafasi ya kuwa sehemu ya kujenga uchumi wa viwanda ikiwemo kulima kilimo endelevu kwa kuangalia mahitaji ya soko ndani nan je ya nchi. . Kenya wametangaza, njaa kutokana na changamoto za mabadiliko ya tabia nchi. Somalia wametangaza njaa. Djibout na Sudan hali kadhalika. Wingi wa watu hawa wanahitaji chakula. Tanzania tuna fursa ya kufanya kilimo endelevu cha umwagiliaji. Tuna fursa ya kuvuna na kusindika mazao ya chakula na mazao malighafi kwa viwanda ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje.
Barcelona waliamini na kutumia jitihada zote ili kuweka historia. Nasi tuna nafasi ya kuamini na kufanya mambo ya maana. Glenn hakutarajiwa hata kutembea. Ushauri wa daktari ilikuwa ni kukatwa miguu. Miguu ya Glenn, maishani mwake iliweka rekodi kadhaa si za kukimbia kama mimi na wewe ambao tunaweza kukimbia si kwa mashindano, bali Glenn alivishwa medali katika mashindani makubwa kama Olimpiki ndani na nje ya nchi yake.

Watanzania tunawajibika kuamua. Tunaweza kuwa-prove wrong wale wasio amini na watazamaji. Nchi za Asia ya mbali miaka ya 60 zilikuwa kama sisi katika hali ya kiuchumi. Asia waliamua kwa juhudi zote na leo baadhi ya nchi hizo wanatusaidia kiutaalamu, kutuunzia vitu na mambo chungu mzima.

Ni wakati wa kuamini na kutenda kwa kupigana mpaka mambo yatokee. Barcelona hawakuwa na muda wa kumlaumu kocha Luiz Enrique. Wachezaji walicheza mpira ili kuleta matokeo. Watanzania tunawajibika kucheza mpira wa kuwa sehemu ya maendeleo ya Viwanda. Tukiweza kukuza kundi la wazalishaji bila shaka kundi la walipa kodi litakuwa na kuongeza makusanyo ya hazina.

Kwa pamoja tunaweza kujienga Tanzania.  

Fred Matuja
fmatuja@hotmail.com  
 



Tuesday, March 7, 2017

RAIS MAGUFULI ANATUTAKA TUSOME KITABU CHA DONALD TRUMP




The beginning of every government starts with the education of our youth.
(Mwanzo wa kila serikali unaanza na kuwapatia elimu vijana wetu)
—Pythagoras


Katika kitabu chake cha “Think Like a Champion” yaani fikiria kama mshindi, mwandishi Donald J. Trump ambae kwa sasa ni Rais na Amri Jeshi mkuu wa taifa tajiri na nguvu za kijeshi la Marekani, amenukuu falsafa ya Pythagoras.


Muandishi Donald Trump, amehimiza umuhimu kwa kujifunza na kuoanisha aina ya kujifunza kama mwanzo mpya kwenye kila zama ambayo mtu unaingia. Katika kitabu hicho Donald Trump ameonesha jinsi Pythagoras aliekuwa nguli wa falsafa hususani katika somo la hisabati, mara nyingi alitafsiri mambo mengi kwa kuoanisha au kuwakilisha na tarakimu au nambari.


Donald Trump yeye kama mfanya biashara nyakati ameandika na kupiga chapa kitabu kicho yaani mwaka 2009 ameonesha kuwa kuna muunganiko wa moja kwa moja kati ya elimu inayompa mtu mmoja mmoja maarifa hali kadhalika jamii nzima kupata maarifa kupitia mifumo mbalimbali ya elimu.


Mie ninaendika makala hii kwa uzoefu na ujuzi niliopata wakati nasoma chuo cha ualimu na baadae kupata mafunzo ya taaluma nyingine, naweza kurejea jambo ambao nimewahi kuandika huko nyuma kuwa sisi wanadamu, tuna namna ya kujifunza shule au vyuoni (formal education), kuna namna ya tunajifunza kwa malengo maalum ili kupata ujuzi tunaoutaka (non-formal education). Vilevile tunaweza kujifunza kwa kupitia vitabu, majarida, mitandao ya kijamii, program za radio, televiseni n.k na hii inaitwa (informal education). Vyovyote vile, maarifa tunayoyapata yanatakiwa kutubadilisha namna ya kufikiri na kuzalisha mabadiliko ya kitabia.


Trump, alijikita katika kusisitiza kila mtu anapoanza jambo jipya, kuna umuhimu wa kujifunza au kujiongezea maarifa mapya kuhusiana na mambo mapya anayotaka kuyafanya. Mwandishi ambae ni Rais wa awamu ya 45 kwa sasa ya Marekani amejielezea kwa uzuri namna ambavyo amekuwa katika kujifunza ujenzi wa nyumba na hoteli ili anapokuwa na wahandisi-wajenzi walau asiachwe nyuma na lugha za kimsingi za kiufundi hasa katika ujenzi.


Kuna nyakati alijikita katika uendelezaji wa viwanja vya gofu, ilimlamlazimu pia atafute kundi la wataalamu wa kucheza mchezo wa gofu na wajenzi wa viwanja wa gofu. Lengo lake, ilikuwa ni kukaa na wataalamu kwa lengo la kupata taarifa za msingi kutoka kwenye uzoefu wa sekta au biashara ambayo alikusudia kuifanya.


Donald Trump aliamini na anaamini sana katika hisia mpya huwa zinajengwa katika misingi ya mwanzo mpya na mwanzo mpya umeunganishwa na maarifa mapya yanayopelekea namna mpya ya kufikiri na namna mpya ya kutenda ili kupata matokeo mapya.


Haina tofauti na msemo wa kibiblia wa umuhimu wa divai mpya katika chupa mpya ili kupata matokeo tarajiwa. Tofauti na divai mpya unaweka katika chupa ya zamani. Inapelekea kupoteza divai na chupa hali kadhalika.


Natamani kununua au kuazima uzoefu wa falsafa ya Donald Trump katika muktadha wa Tanzania ya Rais John Pombe Magufuli na Watanzania walio wengi.


Kuna namna Mheshimiwa Rais ameingia darasani kama mwalimu na anatoa mafunzo kwa chaki ubaoni. Wakati Mwl. Magufuli anafundisha kwa mujibu wa mungozo mpya wa somo (new syllabus) kwa upande mwingine wanafunzi ambao ni Watanzania wanakumbuka mafunzo na malezi ya Mwl. Jakaya Mrisho Kikwete ya awamu ya 4. Na wengi wakitaka kuishi kama awamu ya 4.


Falsafa ya Mwl. Kikwete ilikuwa 1+ ( ) = 5. Wanafunzi ambao ni Watanzania tulikuwa na jukumu la kufikiri ni namba ngapi ikijumlishwa na moja tunapata 5. Kwa muongozo wa kujifunza haukuhitaji njia ya kuonesha jibu ambalo ni 4 umelipataje. Na kwa muongozo wa mafunzo yale, ukiweka 4 mwalimu atakupa vema kwa kuwa jibu ililoweka ni sahihi.


Mara hii ameingia Mwl. Magufuli ambae ana swali kama lile la mwalimu wa awamu ya nne, isipokuwa badala ya parandesi, wakati swali lina herufi X
1+X = 5.


Mwalimu Magufuli anataka utafute thamani ya X kwa njia za kihisabati za jiometri.


Sote tunakubaliana kuwa thamani ya X ni 4, isipokuwa njia ya kuifikia 4 ni tofauti na muongozo wa mafunzo ya Mwl. Kikwete.


Awamu ya 5 anatutaka ili kupata jibu, sisi Watanzania ambao ni wanafunzi darasani, tuna wajibu wa kujua kwamba tunatakiwa kuonesha njia ya kulifikia jibu ambalo ni 4.


Kwa lugha rahisi inatakiwa kuchukua swali 1+X = 5 na kutoa 1 kila upande


1+ (-1)+ X = 5 – 1


Jibu litakalopatikana litakuwa wazi kabisa kuwa


0 + X = 4


Hivyo basi kumbe thamani ya X = 4.


Huu ndiyo mfumo wa muongozo wa mafunzo anayotumia mwalimu wa awamu ya 5. Kuna uwezekano kutokana na wepesi wa masomo awamu ya 4, kuna nyakati mwalimu alihitaji tuimbe nyimbo kama sehemu ya kujifunza.


Isipokuwa muongozo wa kujifunza na kufundishia uliopo sasa watutaka tujue namna tofauti ya kutafuta thamani ya X. Muongozo wa mwalimu hautupi fursa ya kuimba kama namna ya kujifunza kama kule nyuma. Na hapa ndipo tofauti inapoanza kuonekana kwani baadhi ya wanafunzi bado wanatamani uji kumbe tupo katika zama za kula ugali na nyama ya mifupa. Tunawajibika kutumia meno yetu kutafuna kuitoa nyama katika mifupa.


Wanafunzi darasani (yaani Watanzania wengi) bado wanataka mwl. Magufuli afundishe kama mwl. Kikwete na kutumia njia za zamani kuja na jibu la thamani ya X.


Nitoe rai kwa Watanzania wenzangu ambao ni wanafunzi katika darasa la mwalimu wa awamu ya 5; chonde chonde, tuna jukumu moja kubwa la kufanywa upya namna ya kufikiri. Namna pekee ya kufikiri na kukubaliana na ukweli, mfumo mpya wa muongozo wa mafunzo ndivyo unavyotaka, na mwalimu tulie nae, muongozo wa masomo na mbinu zake za kujifunzia si kuimba (nibebe nibembeleze kama wimbo mmoja uliowahi kutamba katika nyimbo za injili).


Tukiji-position kwa kujua tupo awamu ya 5 na kuamua kujikita katika mbinu mpya za kukokotoa ili kupata majibu; tukifanya hivyo bila shaka lawama na manung’uniko yataisha. Na tutajikuta tunawajibika na kujituma kwa kutumia mbinu halali na njia halali ya kufikia jibu.


Tukigoma kujifunza, tunajiweka katika hali ya kutokua kiufahamu hususani kwenye kukabiliana na changamoto zinazotuzunguka.


Tunaweza kupata jibu la changamoto nyingi ikiwemo kutengeneza hela kihalali bila kutumia njia za mkato pale tu tunapojua, awamu hii na muhula huu, unahitaji mtanzamo mpya katika utatuzi wa matatizo yanayotuzunguka.
Na utatuzi unapofanyika, maana yake njia ya kufikia jibu inatakiwa kuwa wazi ili mtu yeyote anaekagua namna mwanafunzi alivyopata jibu, bila maswali ya ziada aone jibu lilivyopatikana.


Ili tufaulu hisabati za mwl. Magufuli hatuna budi kumpenda na kumkubali kuwa ndiye mwalimu wetu na tunawajibika kukubaliana na mbinu zake za kufundishia na kujifunza ili kupata matokeo tunayotarajia.


Wataalamu wa saikolojia wanaonesha kuwa, wanafunzi hufaulu vyema pale wanapokuwa na uhusinaano mzuri na mwalimu huhusani kwa kumpenda na kushirikiana nae hata nje ya saa za darasa kwa kwa nia njema ya kujifunza ili kutatua mafumbo kwa lengo la kupata majibu.


Chuki kwa mwalimu hupelekea kuchukia somo vilevile, na hatimaye kushindwa kukabili changamoto za masomo. Ufaulu wa masomo ni faida ya mwanafunzi kupata daraja zuri au alama nzuri. Ufaulu wa kutatua changamoto zinazotuzunguka, sisi wanafunzi (Watanzania) ni wafaidika wa kwanza.


Hii yanikumbusha siku chache zilizopita nilipata kuhudhuria mafunzo yaliyokuwa yakifanywa na maafisa wa kijeshi. Moja ya kitu nilichopata katika mafunzo yale, ni namna wapiganaji hao wanavyofikiri ili kupata majibu ya utatuzi wa maswali magumu au changamoto mbele yao.


Afisa mmoja akatoa mfano, ukikutana na mto wenye mamba wakali na unatakiwa kuvuka upande wa pili wa mto; Je utapita katikati ya maji ili mamba wakutafune au utafanya nini. Afisa yule wa kijeshi akaweka wazi kuwa, kuna namna ya kuishughulisha akili ili kupata suluhisho la kusonga mbele na kuendelea na safari ili kufika kule unakotaraji.
Moja ya suluhisho lililotolewa na mpiganaji yule ni kurusha kamba upande wa pili wa mto na kuifunga kamba nyingine kwenye kipago au mti mubwa na kisha kuvuka kwa kutambaa kwa miguu na mikono kwenye kamba huku mamba wakikukodolea macho unapopita juu yao.


Kwa mtu mwingine angeweza kurudi alikotoka, mwingine angeweza kutupa lawama ooh… kuna mamba kwenye mto, na mie siwezi kuvuka. Tofauti ya kufikiri kwenye tatizo lile lile ndilo linawafanya Wanajeshi kujiona washindi na akili zao zimejiengwa kusonga mbele hata pale mambo yanapokuwa magumu. Hivyo kurusha kamba upande wa pili na kisha, anavuka kwa kamba ni moja ya mbadala katika mbinu mpya ya kutatua tatizo la mto wenye mamba.


Katika nyakati hizi, tuna wajibu wa kufikiri kwa kiwango sawia na muongozo wa somo la awamu ya 5. Moja ya assignment (homework) aliyoitoa mwalimu Magufuli wakati mmoja akiongea na wahariri, ni waandishi kufungua kampuni ili kujenga viwanda au kuwa na shughuli ya uzalishaji mkubwa unaotoa ajira kwa vijana na kuongeza thamani ya malighafi hasa za mazao ya kilimo na mifugo. Nae Mheshimiwa Rais alitoa ahadi ya kusaidia mchakato ili kampuni hilo lipate mkopo kutoka benki ya ukekezaji. Je kuna, mtu au waandishi wameshapeleka andiko la mradi wa kampuni na mwalimu wetu wa darasa la awamu ya 5 akashidwa kutoa msaada? Au ndiyo wengi wanatumia kalamu na keyboard za social media kulalamika tu?


Kumbe tunaweza pia kungusha mti na kuulaza upande mmoja wa mto kwenda upande mwingine na kuvuka kwa kutambaa juu ya gogo la mti na kuendelea na safari ya maisha pasi kulalamika kwanini mwalimu anatuelekezea njia ngumu za kupata matokeo.


Mungu ibariki Tanzania. Tuna jukumu la kumkubali mwalimu wetu ili tufaulu mitihani katika zama za mafunzo mapya ili kupata alama nzuri na kusonga mbele katika hatua ijayo.


Fred Matuja

fmatuja@hotmail.com

Wednesday, February 15, 2017

I have found a new friend...





This young one was left to live in our compound by her mother some few days after she was born. We decided to take care of her and it is some few months down the line and she is becoming a part of our family. She is very charming and playful, she recognizes the sound of our car and run very fast to say welcome home every evening.

My boys have decided to call her Tomtom. She is a good firend

Friday, February 10, 2017

Nice rain shots




Nimekutana na mama Elizabeth Bhoke!

 Katika maisha kuna wakati huwa unaweza ukapata changamoto sana na ikakufanya ujiulize na ujichunguze Imani yako kwa Mungu. Kuna watu wanampenda Mungu sana na maisha yao wamejitoa kwa Mungu kwa asilimia zote. Sasa hii changamoto ndio niliyokutana nayo.

Nimekutana na huyu mama anaitwa Elizabeth Bhoke. Mama huyu ana umri wa miaka 79 na hana mume wala mtoto lakini yeye ni mwinjilisti ambaye huzunguka akikusanya Pesa ili ajenge makanisa katika wilaya ya Serengeti. Mama huyu wa kanisa la Sabato, tayari amejenga makanisa matano huko Serengeti na anaendelea kukusanya pesa ili kujenga mengine.

Huu ni moyo wa ajabu sana sana na kwa kweli umenipa changamoto sana ya kumpenda Mungu zaidi na kujali kile ambacho Mungu amekiweka ndani yangu na kukifanya kwa bidii sana kama huyu mama.

Kama mama huyu atakufikia tafadhali nyosha mkono wako na umbariki. Yeye pia hutoa maneno ya kubariki sana na pia ni mchangamfu mwenye maneno mengi ya kutia moyo....



Im so challenged!. God Bless you mama!

Thursday, February 9, 2017

PAULO MAKONDA NAOMBA UJIFUNZE KWA SIR NICHOLAS WINTON


Nicholas Winton
Ilikuwa mwaka 1938 wakati kijana mdogo wa miaka 29 aliejulikana kama Nicholas Winton ambae aliekuwa ni dalali wa hisa (stockbroker) jijini London aliamua kuacha shughuli zake na kwenda nchini Czechoslovakia. Lengo la safari yake ilikuwa ni kuwaokoa watoto wa Kiyahudi 669 waliokuwa katika kambi ya wakimbizi.

Nicholas alitengeneza mpango wa kuwavusha kutoka Czechsolovakia na kuwapeleka watoto hao England; alipofika England alifanya kazi ya kutafuta familia za Waingereza na kuzishawishi ziwachukue watoto hao kwa lengo la kuwalea.

Katika mpango huo kabambe, Nicholaus alichukua magari 8 na kwa umakini na usiri mkubwa alifanikisha zoezi hilo la kuwaokoa watoto hao. Nicholaus alifanya siri ambayo hata mkewe hakuweza kujua. Miaka 50 baadae, mkewe wakati anapekua pekua vitu, aliweza kuona kitabu kikiwa kimefichwa kwenye dari. Kitabu hicho cha similizi kinachojulikana kama (scrapbook) kilikuwa na majina na picha za watoto wote waliokolewa na Nicholas kwa takribani miongo 5 iliyopita. Mkewe, Greta aliamua kuichukua simulizi hiyo na kumpelekea Elisabeth Maxwell ambae alikuwa mtafiti wa mauji ya kimbari ya Wayahudi (Holocaust) na barua za hao watu waliokuwa watoto nyakati hizo. Kulikuwa na mwitikio kutoka kwa watu zaidi ya 200 kati ya wale 669 katika ile orodha ya watoto kwa miongo 5 iliyopita kwa wakati huo.

Dunia iliyobakia nikiwemo mimi nawe msomaji wangu ilikuja kuifahamu simulizi hii kupitia filamu-simulizi (documentary) iliyotengenezwa na kituo cha habari cha BBC yenye jina That’s life (yaani haya ndiyo maisha). Nicholaus alialikwa kama mmoja wa wahudhuriaji wa katika onesho hilo. Kile kitabu chake cha kumbukumbu kikafunuliwa na maelezo kutolewa, na aliekuwa mwenyeji wa hafla hiyo akauliza umma uliokuwa umehudhuria ambao walikuwa wameokolewa kutoka na uamuzi wa Nicholas kuokoa maisha yao. Zaidi ya watu 20 walisimama wakiwa wamemzunguka Nicholas na kupigia makofi ya kumpongeza na kumshangilia Nicholas.

Waweza kuiona video hiii kupitia tovuti ya www.youtube.com/watch?v=6_nFuJAF5F0 na kumwona mtu mkuu alieamua kugusa maisha ya watu na vizazi vingine baadae maishani. Kwa uchache kati ya watu aliowaokoa ambao ni maarufu katika jamii ni pamoja na Alf Dubs, Baron Dubs (iliezaliwa mwaka 1932) na alikuwa Mbunge wa bunge la Ungereza kwa kupitia chama cha Labour. Heini Halberstam (aliezaliwa mwaka 1926) na alikuwa bingwa wa hisabati. Renata Laxova (aliezaliwa 1931), alikuwa daktari bingwa wa masuala ya vinasaba vya watoto (peadiatric geneticist). Wengine ni Joe Schlesinger (aliezaliwa 1928) alikuwa mtangazaji wa vipindi vya televisheni huko Canada na muandishi wa vitabu. Na wa mwisho kumtaja katika makala hii katika orodha ndefu ni Yitzchok Tuvia Weiss (aliezaliwa 1926), alikuwa Rabi Mkuu Jerusalem. Rabi ni mwalimu wa dini ya kiyahudi.

Mpaka mwaka 2015 shirika la habari Uingereza BBC liliweza kuwasiliana na zaidi ya watu 200 kati ya waliokuwa watoto 669 walioweza kuoka na zahma la mauji ya kimbari.

Kutokana na maamuzi aliyoyafanya Nicholas, amefanikuwa kukusanya tuzo za heshima chungu nzima ikiwemo kupewa cheo cha heshima na ushujaa kutoka kwa malkia Elizabeth II wa na kuwa SIR NICHOLAS WENTON. Jamhuri ya Czech ilimpa Sir Nicholas Wenton tuzo ya heshima ya Simba Shujaa; Kwa upende wake Rais wa awamu ya 7 nchi Israel Ezer Weizman aliwahi kumpa tuzo ya heshima kwa niaba ya Taifa lake. 

Nimeguswa sana na watu wengie pia wameguswa na maamuzi ya Nicholas aliemua kuhatarisha maisha yake na kutumia gharama zake kwenda katika kambi kwa lengo la kuokoa watoto ili mkono wa mauaji ya kimbari wa Adolf Hitler usiwafikie. Miaka 50 baadae simulizi hiyo iliwekwa wazi na watu wengi kujua juhudi na “innitiatives” za Sir Wenton alizofanya akiwa kijana mdogo.

Napiga picha ya initiative ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Ndugu Paulo Makonda ya kunzisha vita dhidi ya uuzwaji wa dawa za kulevya jijini Dar es Salaam. Kimsingi watu wengi wamepokea taarifa hii kwa mshangao kuna kwamba “atafika wapi!”

Aidha kuna wengine wanamkejeli kama mtu anaejaribu kufunika aibu ya wanafunzi wa kidato cha nne kufeli hususan mkoani Dar es Salaam. Wengina wakidhani anatafuta umaarufu. Kila mmoja kwa hisia zake.

Binafsi nampongeza Paulo Makonda kwa nafasi yake na uzalendo wake kwa nchi uamuzi wa kuchukua hatua ya kufanya uchunguzi kwa kushirikiana na vyombo vilivyo chini ya ofisi yake na kutoa amri ya watuhumiwa wanaohusika kukamatwa ili wahojiwe na wengine kusimamishwa kazi ili uchunguzi uendelee pasipo wao kuathiri uchunguzi kama watakuwa kazini.

Nia ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ni njema. Amenuia kupiga vita vizuri dhidi ya biashara ambayo inaua hatima ya vijana wa Kitanzania. Tukumbuke matokeo ya vijana kutumia “unga” ni kuwaharibia kesho yao na mchango wao ambao wangeweza kuutoa katika ujenzi wa taifa hili.

Ilitakiwa Watanzania kwa nafasi zozote tulizonazo tusimame na Paulo Makonda kwa kuwa anachokipinga ni kitu kibaya. Michelle Obama wakati mmoja aliwahi kusema kuwa “kumpiga vita mmoja wetu ni kutupiga vita sote” Kwa mantiki hiyo kumpiga Paulo Makonda nia yake njema ni kupinga sheria za nchi zenye lengo la kuzuia matumizi, uuzwaji na usambazaji wa madawa ya kulevya.

Ni ukweli ulio wazi kuwa, mtu yeyote mwenye mguso maishani alijengewa mazingira mazuri ya kumsaidia kufika ndoto zake maishani. Mihidarati ni kitu ambacho kinaweza kuharibu tabia njema na mwenendo wa vijana na watoto kuifikia kesho yao. Hivyo basi tunawajibika kuipingwa kwa ngivu zote.

Yawezekana si kila mtu ana nafasi ya kuwa kwenye vyombo vya dola ili kutumia misuli kuzuia utumiaji wa mihadarati au usambazaji; kutokuwa na nafasi kama ya Paulo Makonda au IGP Ernest Mangu, bado tuna jukumu la kupigana kwa kupitia kuwatia moyo wapiganaji walio-mstari wa mbele kwa njia ya kuwaombea kwa Mungu au hata kupaza sauti kupitia vyombo vya habari. Na tukiachukulia mfano wa wapenzi wa soka anafahamu nguvu ya kumshangilia mchezaji au wachezaji wanapofanya vizuri.

Nicholas alifanya maamuzi ya kuokoa watoto 669, miaka 50 baadae, watu wale walikuwa watu wenye mguso akiwemo muandishi wa habari, daktrari bingwa wa watoto, mwalimu mkuu wa dini na wengine wengi. Juhudi za Makonda zikifanikiwa Dar es Salaam na kila mmoja akacheza nafasi yake kutimiza wajibu wake kukaba ili wasambazaji wasiendelee kuuzaa katikati yetu, ni watu wangapi tutawaokoa?
Kama Mtanzania mzalendo, sioni kama mihadarati ina nafasi ya kuongeza thamani katika maisha ya watoto na vijana kama wahanga wakubwa wa mihadarati.

Rai yangu ni kuwa sisi kama wanajamii tunawajibika kwa pamoja kuijenga nchi hii. Jirani akiharibikiwa au mtoto wa jirani akiharibikiwa madhara yake yana uwezekano kwa upande mmoja au mwingine kugusa maisha yangu au watoto wangu. Njia rahisi ni kuamua kupigana kuzuia madhara yasisambae kuliko kuachilia yasambae.

Rais John Magufuli kampongeza IGP Mangu kwa kuchukua hatua ya haraka za kinidhamu kwa watuhumiwa ndani ya Jeshi la Polisi ili kupisha uchunguzi ufanyike.

Tukipanda mbegu njema kwa kugusa maisha ya wengine, ipo siku tutavuna taji ya heshima kwa mrejesho wa watoto wetu na vijana wetu kuwa na mguso chanya kwenye jamii. Ili jamii yetu iwe na uzalishiaji wenye tija (effective production) mihadarati lazima ipigwe vita ndani ya mipaka yetu. Paulo Makonda kaonesha mfano, kwa pamoja tumuunge mkono.

Fredrick Matuja
fmatuja@hotmail.com

Note: Tunamshukuru sana Fred Matuja ambaye amekuwa akitutumia makala ili tushirikiane na wadau mnaopitia kwenye blog yetu.