Tafuta/Search This Blog

Tuesday, August 28, 2012

Papaa On Tuesday......Maisha Ya Pembe Tatu Ni Kwazo la Maendeleo Kwa Mkristo-2

 

Niwasalimu Kupitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo.

Wakati Zoezi La Sensa Limeanza nilibahatika kuhesabiwa siku ya Jumapili na kwa dakika zisizozidi 10 nilishaongea mengi na aliyekuwa Karani Wa Sensa Kwenye Nyumba yetu. Kati Ya Mambo tuliyoongea kidogo ni Mfumo wa Maisha tuliyoamua kuishi Watanzania am Wakristo Kwa Ujumla Wao. Na Katika Mazungumzo nilikuja baini kumbe Jamaa ananifahamu na ni Msomaji Mzuri wa Blog Hii akanikumbusha Papaa On Tuesday ambayo ilimbadilisha namna ya Kuwaza ambayo ilibidi niisome tena siku ya Jumapili Usiku kuona kile ambacho kiliandikwa mwaka Juzi kilikuwa ni nini hasa.

Niwashukuru Wasomaji wa Blog na Marafiki wa Facebook waliokuja kwenye Presentation Ya Papaa On Tuesday niliyofanya Live Pale VCC Jumamosi hii ya 'Think Differently and Make a Difference". It was Awesome sana Mungu awabariki.

Kati ya Mambo unapaswa to think Differently and Make a Difference ni mfumo wa maisha ya pembe tatu tunayoishi nikiwa na maana, 1. Unapolala (Nyumbani) 2. Unapofanya shughuli zako (Kazini ama shuleni) 3. Unaposali (Kanisani ama Fellowship).Kuna watu wakiamka asubuhi wanajiandaa kwenda kazini ama darasani, wakitoka wanaenda labda kanisani ama fellowship kisha wanarudi nyumbani kulala, kesho yake wanaamka wanarudia mzunguko huo huo.

Nichangamoto kubwa sana ya kizazi hiki ambacho kila mtu anataka kuwa "mjasiriamali" wa namna moja ama nyingine ama mtu unakusudia kuongeza kipato chako cha fedha then una maisha ya pembe tatu. Mtu yeyote unayemuona either amefanikiwa kwa namna moja ama nyingine lazima huyu mtu anamizunguko zaidi ya hiyo uliyonayo. Usitafute mchawi mchawi ni wewe mwenyewe.
Siku Moja Swahiba Prosper Mwakitalima aliniambia niambia "Hakuna tusi baya kama kusema haiwezekani, then ukakuta kuna mtu amefanya". Kati ya vitu ambavyo tunavyo na hatupendi kuvitumia ni ubongo, mfumo wa makuzi na malezi tuliyokulia umetusababishia mtu mwingine awaze kwa niaba yetu sisi tuchukue mawazo yake, huwezi kuwa msomi mwenye akili za kutosha na ubunifu wa hali ya juu kwa kutegemea "madesa", notes za handout na past papers, ndio maana waliokuwa wazuri "kukariri" darasani kwenye maofisi huku ni wengine ni vituko. Mimi ni mwandishi lakini nina taaluma yangu,ninapoandika na kusababisha hii Blog iwe na mambo ya maana iwe current sio sababu ya maombi, sababu kubwa am working hard for this, nachelewa kulala sababu ya kuwaza, inanipasa kusoma sababu ya hii, inanigharimu muda ili wewe usome, inanigharimu fedha ili mtu mmoja apone, we will never be the same my dear. Chukia mizunguko mitatu kwenye maisha yako.

Unaweza pata wapi mawazo ya biashara kwa maisha ya pembe tatu, unaweza pata wapi wateja ama network ya watu kwa maisha ya pembe tatu, unaweza fanya jambo gani kwenye Jamii kwa maisha ya pembe tatu??kila utakachokuwa unaongea ni Kazini kwetu, Kanisani kwetu, kwenye TV kwenye nini sijui...Wake Up. Kwa taarifa yako kuna watu wa rika lako wanafanya mambo makubwa wewe ukiwa bado unawaza nini cha kufanya. Kuna wanafunzi kama wewe wameanza kujiongezea kipato chao, kuna wafanyakazi kama wa ngazi yako hawategemei mishahara yao..tatizo kubwa sisi tukitoka kazini haooooooo, kanisani, tukitoka kanisa haooooooo kulala, get me well kuna wengine hata maofisini mwao ama shuleni ama vyuoni mwao ama kanisani kwao hawaoni kama hao ni Opportunity kwenye maisha yao.

Kuna wengine mpaka sasa hawajaoa wala hawajaolewa si kwa sababu Bwana hajataka ila Mfumo wao wa maisha una walostisha, kuna wengine mpaka sasa hawajapata kazi si kwa sababu Bwana hajataka ila mfumo wapembe tatu unawalostisha, kuna wengine mpaka sasa biashara ni ngumu sababu ya mfumo wa pembe tatu. Ninaamini tumeumbwa tofauti, lakini through friends ndipo unaweza gundua kile ambacho Mungu ameweka kwenye Maisha yako pia. Aliyenipa wazo la kuwa na Blog is my friend Weda Ringo..she saws something in me akasema Papaa you Can do It, but wote hatukujua on "how to do" kwenye Nia pana njia, leo hii Blog imesimama, Blog imekuwa chanzo changu cha fedha, Blog imekuwa Msaada kwa Watanzania wenzangu na Ulimwengu kwa Ujumla. Blog imekuwa madhabahu ya wengine kufunguliwa. Nilipoanza Blog sikujua kama nitakuwa na "Papaa On Tuesday" lakini Mungu akawapa akaweke idea ya mimi kuwa na "Papaa On Tuesday", leo kuna wazo lingine ninalo ambalo pia litabadilisha mtazamo wa Blog hii, siangalii leo, wala mwaka huu ninatazama miaka mitano ijayo.Na kile Mungu anasema kuhusu Blog hii.This will be the most Popular Christian Blog hapa Tanzania si kwa sababu ya mapicha picha au sababu ya uandishi I came to realise this blog is not mine, last week nimepokea testmony za kutrosha mpaka nikaogopa kuwa kupitia Blog hii kuna watu wamepona kabisaaaaaa magonjwa yao, kuna watu wanainuliwa kupitia blog hii, kuna watu wanasubiri Jumanne Kusoma Papaa On Tuesday sababu anajua kuna Kitu kutoka Madhabahu hii. Nimejifunza kumsikiliza aliyeniajiri katika kazi hii na kuweka hizi idea na gifts ndani yangu anataka twende wapi kupitia blog. Is not only about writings lakini how many people wamekuwa transformed wamekuwa inspired kupitia hapa, we need to live a life with impact.

Lakini haya yote is not all about me kuna watu wananiombea kuna watu wananipa Ideas. Let me be Honesty Mwanzo ni mgumu sana, na kuna watu wanapenda wengine wafanye wao wanavyodhani ni vizuri, nimekutana na watu wengi sana wanatamani Blog yangu ile kivileeeeeeeee, wengine wanaongea rangi mbaya, wengine wanaongea lugha ninayotumia, wengine wanaongea kuna picha nyingiiiii, the simplest thing that I always do, ninasikiliza then ninachambua kina go ahead ya ndani ama lah kama sio napiga chini wazo kama unaona unaweza anzisha Blog yako iwe inavyotaka kuwa, usikate tamaa kwenye maisha huwezi jua nini kitakutoa kwenye maisha yako.

Ukiona mwezi mzima unamaisha ya pembetatu tafakari kisha chukua hatua. Kila siku ya Mungu lazima nikutane na watu kwa ajili ya kubadilishana mawazo na kila siku ninapata mawazo mapya kupitia watu kupitia vitabu mbalimbali.

Think Differently and Make a Difference.
...//Papaa
0713 494110
samuel_sasali@yahoo.com
posted by 0718817706

No comments: