Tafuta/Search This Blog

Thursday, December 30, 2010

Hukumu ya Chenge - MZAHA!!

Sijaamini macho yangu niliposoma habari kuhusu hukumu iliyotolewa na mahakama dhidi ya Mbunge wa Bariadi (CCM) Andrew Chenge a.k.a Mzee wa Vijisenti ambapo licha ya kutiwa hatiani kwa mauaji ya watu wawili na makosa manne ya barabarani,amehukumiwa faini ya SHILINGI LAKI SABA!And as you would have expected,AMELIPA NA KESI KWISHNEY.


Pengine hakimu aliyetoa hukumu hiyo alikuwa hajatoa zawadi ya Krismas kwa bosi wake mpya,Jaji Mkuu Othman.Au pengine hakimu huyo aliona hukumu hiyo ni fursa nzuri ya kutoa salamu za mwaka mpya kwa Watanzania in form of a prank.Au labda hakimu huyo amezingatia kanuni isiyo rasmi inayotawala sheria za Tanzania kwamba wanaostahili kwenda jela ni walalahoi tu,vigogo wanapokutwa na hatia wanapaswa kunyenyekewa kwa kila hali.Na pale inapobidi kutoa hukumu ya "changa la macho",matokeo yake ndio hukumu kama hii aliyopewa Chenge.


Ungetegemea mtu kama Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Werema kukata rufaa dhidi ya hukumu hii ya mzaha.Lakini atapata wapi muda huo wakati yuko bize kuhakikisha majambazi wa Dowans wanalipwa mabilioni yao?Na ungetegemea makundi ya haki za binadamu yashikilie bango hukumu hii lakini you and I know better kuwa generally speaking civil society Tanzania ni imegeuka mradi kwa wajanja (wezi?) kuwaghilibu wafadhili waendelee kumwaga misaada,ambayo kwa kiasi kikubwa inachangia kuongeza idadi ya mahekalu,magari ya kifahari na nyumba ndogo za wenye NGOs hizo.


Ukiwa Mtanzania,unapaswa kuielewa vema Tanzania.No,simaanishi utafute vitabu vya Jiografia,Historia au Elimu ya Uraia kuhusu Tanzania.Ninachomaanisha ni kwamba unapaswa kuishi katika uhalisia na kufahamu kwamba kuna Tanzania ya aina mbili: ile masikini ya kupindukia ya walalahoi,na ile ya wenye ma-Vogue,X8,Hummer,nk.Pia kuna Tanzania ya wezi wa kuku wanaozeekea jela wakati uchunguzi unaendelea,au wanaobambikiwa kesi kwa vile hawamudu kuwahonga polisi mafisadi,na Tanzania ya akina Chenge ambao hata wakigonga na kuua kwa magari yenye bima iliyoisha muda wake wanaishia kupewa faini ya kishkaji la shilingi laki saba!Pia tuna Tanzania ya wanausalama kuhaha huku na kule (huku wakitumia mamilioni ya fedha za walipa kodi) kuandama maisha binafsi ya wanasiasa kama Dokta Wilbroad Slaa,na ile Tanzania ya wanausalama wanaotweta kuhakikisha mmiliki wa Kagoda anaendelea kuwa SIRI KUU.Na tuna Tanzania ambayo ni haramu kuandamana kudai Katiba mpya au kumpongeza mbunge wa chama cha upinzani,na ile ambapo kauli yoyote ya kiongozi wa CCM (hata kama ameitoa ndotoni au akiwa chakari baa)inageuzwa wimbo wa Taifa.


Inachukiza kuona miaka 49 baada ya uhuru wetu,Tanzania inazidi kugeuzwa punching bag na shamba la bibi la mafisadi.Ufisadi unatapakaa kila kona.Na mahakama zetu hazitaki kuachwa nyuma katika mchezo huo mchafu.Ndio maana sikushangazwa na kauli ya kitoto ya Jaji Mkuu mstaafu Agostino Ramadhani kuwa baadhi ya hukumu za majaji zina walakini (na alisubiri astaafu kwanza kisha ndio atoe kilio.Nchi ya rambirambi!).Actually,Jaji Ramadhani alipata fursa adimu ya kuingizwa kwenye vitabu vya historia pale aliposhiriki katika hukumu ya mgombea binafsi.Lakini tungetarajia nini kuyoka kwa wateuliwa ambao utiifu wao uko zaidi kwa aliyewateua kuliko nchi wanayoitumikia?


Nimalize kwa maneno makali.Kuna roho mbili za Watanzania wasio na hatia zilizopelekwa kaburini na Chenge.Kwa lugha nyingine,Chenge alijikabidhi jukumu la Ziraili mtoa roho.Hakimu aliyetoa hukumu hii ya mzaha anafahamu fika kuwa haki haionekani kutendeka japo imetendeka katika hukumu hiyo ya kihuni.Mungu atawalaani washiriki wote katika suala hili.Atawaadhibu ipasavyo kwa kupuuza thamani ya maisha ya marehemu hao wawili.Yawezekana huko waliko wanateseka kusikia thamani ya uhai wao ni shilingi laki saba (inclusive of makosa mengine ya Chenge).Of course,hata kama Chenge angehukumiwa fedha zote za akaunti yake huko Jersey isingetosha kufidia maisha ya marehemu hao,lakini alistahili japo kifungo cha muda mfupi.Lengo la hukumu kali ni kutoa fundisho kwa wazembe na wahalifu.Huruma au mzaha kwa wavunja sheria inachangia sana kukomaza uvunjaji sheria.Ikumbukwe kuwa hukumu hiyo inaweza kutumika katika kesi nyingine kuepisha adhabu kali kwa dereva mwingine atakayegonga na kuua ( hususan kama anatoka Tanzania ya vigogo).


Ee Mola,wewe ni mwenye huruma na mtoa haki ya kweli.Blogu hii inakuomba utoe hukumu mbadala ambayo angalau itaweza kuonyesha kuwa haki sio tu imetendeka bali pia inaonekana imetendeka.Katika Wewe kila jambo linawezekana.Kwa Chenge na hakimu wako,kwa hakika ipo siku mtavuna mlichopanda katika mzaha wenu huu wa mwisho wa mwaka!

- Chahali.

Tuesday, December 21, 2010

UKIPENDA BOGA UPENDE NA UA LAKE.


Nadhani wote tumesikia kuhusu mgomo wa wanachuo wa chuo kikuu cha Dodoma juzi na jana. Mimi kwa upande wangu sikutegemea chuo ambacho kipo kwenye mjengo wa chama Tawala kuna siku watagoma na kuona mabaya ya chama "chao".
Nimeshangaa sana kwamba hawa wanaharakati ambao wiki chache zilizopita waliishangilia serikali mpya na waliunda kwaya wakati wa kampeni kumsapoti mkuu, na pia waliitisha press conference kwa ajili ya kuwasema vibaya wanaharakati wa CHADEMA walipotoka nje ya bunge kwa ajili ya kudai haki za msingi za wa Tanzania, leo na wao wamezinduka! Hahahaa mmechelewa sana wadogo zangu. Itisheni tena basi ile press conference labda watawasikiliza tena wakati huu mnapokuwa kinyume nao!!
Mlidhani mtavuna nini baada ya kupanda bangi?? Haya tunawasikiliza kwa furaha sasa.
Namalizia na haya maoni yaliyotolewa na wadau wa website ya Global Publishers kuhusu habari hii nikayapenda sana;


"Teeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeh! tuliwaonya UDOM yakowapi sasa. Siyo nyie mlio kuwa mstari wa mbele kuchangia pesa kwa ajili ya kuchukulia fomu mheshimiwa, na siyo nyie mlioandika barua ndefu mkilaani yaliyotendwa na CHADEMA. mlidhani mtapewa kipaumbele kikubwa au kuwa mambo yatabadilika, hapo mtasoma plate number. Mkumbuke kuna deni la dowans na madeni ya pesa za kampeni, zote zinatakiwa zirudishwe. Hilo ni trela bado miaka 4 na miezi kadhaa, itawagharimu sana. Hiyo ndo raha ya kurupuka bila kupima na kuropoka. vumilieni ndo serikali mlioitaka. Tchaoooooooooooooo ndo maana yake."

****************************************************************************
"sasa ndo mnafanya nini? Mbona na nyie mmemgomea Rais? Au hamjui suala la kuhakikisha ubora wa elimu ni moja kati ya ahadi zake na kama hicho ndo alichowaahidi so mnagomea nini? Nyie U DOM ni waajabu sana tulitegemea wasomi kama nyie ndo mgekuwa mstari wa mbele kutazama maovu ya nchi na kusapoti wanaharakati kama wabunge wa CHADEMA ila ushamba wenu uliwafanya kukurupuka tu, Kweli kunakitu hamkipati kama wanavyuo wenzenu hasa hizo field ndo maana mnajua kuwa hapo chuoni ndo mmemaliza kila kitu. Ondoeni tongotongo kunekucha eh!!!!!!!!"
.

Ndio Zetuuu!

Kuna wakati huwa sielewi kwamba tatizo liko wapi. Kwa mfano kwenye hii picha hapa chini...
Hapa ni ubungo, kuna power plant kubwa na upande wa pili kuna mtambo mkubwa wa kuzalisha umeme kwa kutumia Gas. Lakini ajabu ni kwamba eneo hili liko busy na shughuli za wananchi. Kuna wanaouza mboga na matunda kuna wanaouza mitumba kuna wanaouza DVDs na vitu vingine vingi bila kusahau wanunuzi wao! Sasa mimi hadi sasa hivi sijaelewa kwamba yakitokea maafa hapa tutamlaumu nani?? Tutamlaumu Mungu, au Tanesco kwa kuweka mitambo hapo? au City Council kwa kushindwa kutukataza kufanya biashara hapo? au tutamlaumu mwananchi kwa kununua bidhaa hapo? au labda mtanilaumu mimi kwa kuandika haya??

Nimeamua kumuachia Mungu....

Monday, December 20, 2010

Binadamu Hukutana!


Leo nimekutana na Blogger mTanzania anayeishi Sweden na anaitwa Edina(Pichani hapo juu). Ni jambo la kupendeza sana kukutana na mtu ambaye hukuwahi kufukiri kwamba mtakutana ana kwa ana. tumefurahiana na kwa sasa yupo kwenye ka likizo hapa Arusha.


Wapendwa wadau tafadhali tembeleeni blog yake na inawezekana mkapata bahati ya kukutana naye kabla hajarejea Sweden na hata mlioko huko "mbele" mkakutana kwa pande hizo!


Sunday, December 19, 2010

Tido Mhando Removal's from TBC: Used and Abused

So the infamous Dunstan Tido Mhando is gone!I was a bit shocked to learn that,not because he did or did not deserbe the boot,but rather the fact the the guy had been running TBC as if it were an extension of the CCM-owned Radio Uhuru.You wouldn't blame him,would you?He had to serve his masters in the government who shamelessly disregard the fact that state-run bodies are funded by all Tanzanian taxpayers (minus mafisadi,of course) regardless of their politicwl affiliations.

Tido has simply been used and abused.I'm sorry to say this but anyone,journalists included,who allow themselves to be used by some unscrupulous politicians could find themselves deemed useless once their service is no longer required.We all are aware of how,for instance, our artists attract inexplicable attention from our politicians come elections,only to hear the same cries of "tumesahauliwa" after the elections.Our ever important politicians can't afford to be seen sorrounded by a bunch of wana bongoflava.They had afterall done their job and got paid,so no more reasons for them to hang around with such important people in our society.

Of course we could blame such selfish crooks who never shy away from taking for a long ride whoever willing to attend to their needs but I think the latter deserve a share of such blames simply because they wouldnt be on the receiving end of such dirty games had they resisted being manipulated in the first place.Njaa?kujikomba?Blind faith?or sheer stupidity?

Back to poor Tido,he just reaped what he had sewn.I simply don't get it when I hear some people suspecting that his removal would bring TBC back to the 'Radio Tanzania era'.What they overlook is the fact that before he took the TBC post,Tido was working with one of the best,and hugely transparent,media house in the world,The British Broadcasting Corporation (BBC).Some people.Some of us expected that Tido would have brought "the BBC effect" to Tanzanian media but you and I know how he fared.Of course,I understand it wouldn't have been easy for him to transform an exceedingly biased,pro-ruling party state-owned media into an independent,fair and balanced organisation but at least he could have tried.Praising him for allowing opposition parties candidates to take part in "Jimbo kwa Jimbo" is totally missing the point.Why?Because that's actually what a public funded media organisation is supposed to do.Let us not forget what TBC behaved when Chadema inaugurated their general election campaign.And who was TBC's top boss when that was happening?

Rumour has it that Tido was brought to TBC by a certain bigwig who's currently not in the government.If such rumours are true,then why should we feel sorry for someone who got the job not on merit but rather because someone out wanted Tido at the helm of TBC for the bigwig's personal interests to be realised?

I just hope Tido has learned a lesson that political conmen would never hesitate to use and abuse anyone who is willing to be manipulated.For these cons,any tesource is like a condom: needed before and during sex,but something to disposed of immediately after the act.It's my hope that a decorated professional like him would never again allow any politician to take him for a stepping stone.There were some rumours that a certain fisadi who's aspiring to vie for the presidency in 2015 was planning to recruit Tido as his proposed TV/radio chief.If the rumours eventually turn out to be true in the future,and Tido grabs the offer,then we surely haven't seen the end of saddening chapters in Tido's professional life.

- CHAHALI.

Saturday, December 18, 2010

Tangi J alipopata mwenza wake!

Hayawi hayawi sasa yamekuwa!! Walisema haijai sasa inamwagika!!!
Hatimaye mmoja kati ya wakurugenzi wa SBP kaka Tangi J a.ka Tangibovu amejitwalia mtoto wa kinyasa na kuhalalishiwa mbele ya mimbari takatifu ya kanisa la TAG Kigogo Mburahati Dar Es Salaam. Ilikuwa ni siku iliyofana sana na hatuna mengi maana picha zifuatazo zinajieleza...Mr&Mrs J Lwendo wakiwa na nyuso bashasha za kuanza maisha mapya
Usafiri walioutumia maarusi!


Maarusi wakiwa wamezungukwa na jopo la waheshimiwa wasimamizi na mashahidi. Wote hawa ni ndugu wa Joshua na Happiness.


Vijana wakipigwa maombi ya kuwasaidia kulitunza agano waliloliweka la ndoa takatifu.


Happiness a.k.a Chimwemwe akimvishapete mume wake.

Tangi pia akimvisha pete mkewe.



Maarusi na mashahidi wao. Mr&Mrs J Lwendo na Mr&Mrs G Lwendo.




Kama hapo juu.



Fullu kicheko.


Matumaini.

Wote kwa pamoja.
SPB inawatakia baraka za Mungu katika maisha yenu na Shemeji jiandae kwa ugeni wetu siku za karibuni tutakapokuja kukukabidhi jiko!!

Wednesday, December 15, 2010

BREAKING NEWS!!! OCAMPO'S LIST REVEALED

Ocampo's top six are;
1. William Ruto
2. Uhuru Kenyatta
3. Henry Kisgey
4. Hussein Ally
5. Joshua Arap Sang
6. Francis Muthaura

These are the top suspects of the Kenya's post election violence in 2007.

Sunday, December 12, 2010

Imetimia!!


Ile siku iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu kubwa ya kaka Tangi J (Joshua Lwendo) kumpata mwenzake wa maisha imefika na leo ndio leo. Arusi itafungwa masaa machache yajayo katika kanisa la TAG Kigogo na sherehe kufuata baadae jioni.

SBP itawaletea full report na mapicha ya tukio hilo pamoja na matukio ya send off ya Happiness.

Thursday, November 18, 2010

BREAKING NEWS!!!!!!!

Wabunge wa chama cha upinzani cha CHADEMA, wameinuka na kutoka nje ya ukumbi wa bunge muda mfupi baada ya rais Jakaya Kikwete aliposimama ili kulihutubia bunge la 10.

Wabunge hao wakiongozwa na mkuu wa kambi ya upinzani bungeni ndg Freeman Mbowe waliinuka kimyakimya wakati rais alipoanza kusema neno la kwanza na hali hii iliinua kelele kutoka kwa wabunge wa chama tawala(CCM) ambao kwanza walianza kuzomea na baadae wakaanza kushangilia kwa kusema CCM CCM CCM.

Rais Jakaya Kikwete alionekana kama hajategemea jambo hilo na alikaa kimya kwa mshangao hadi wabunge hao walipomalizika kutoka. Spika Anna Makinda ilibidi kusimama na kuwaambia wabunge waliosalia kutulia na Rais akaanza tena kuhutubia.

Hotuba inaendelea sasa.

Wednesday, November 17, 2010

Facebook haikuanza leo jamani!

Labda ulidhani ni ya siku hizi sana, sasa hebu ona miaka 2000 iliyopita mawasiliano yalikuwa hivi...

Tuesday, November 16, 2010

Stanley Atema Chehe Atangaza Kuanza rasmi Mchakato wa kuaga ubachela

Naitwa Stanley A. Msami

Natangaza kuanza rasmi mchakato wa Kuoa. leo tar 14 Nov 2010


Akimweka Hadharani Mchumba wake Jenifa..Jamani Analipa HAlipiiiiiii?


Analipaaaaaaaaaaaa


Joseph Msami akimpongeza Shemeji/Wifi mtarajiwa (Alimpa zawadi ya Khanga)

Wamama wakimpongeza Mwali (Mwai kwa Kipare)



Wadau wa karibu waliokusanyika.
Haya Matumizi Mbadala hayo ya meno....








Pozi la kukubali kuolewa.


Full figure! Aibu kwa mbaaaaaaaaaaliiii


Mwai pamoja na Mama Mkubwa wa Stanley.



Wazamiaji hawakosagi...


Mwisho Mzee wa familia Mr. Mchome aliomba wadau wafanye Pledge ili kuanza mchakato Mzima wa Harusi. Watu tuliahidi vya kutosha. Natoa wito kwenu wadau kutoa Pledge ili kijana wetu apate jiko. Sio kwa ndugu na Marafiki tu, bali hata wewe.
Wasiliana hapa kutoa pledge 0716176843. Karibu kwa maandalizi.

CHADEMA CHAPEPEZA BENDERA CHINA

Mdau wa blog ya Shalom Broz Elifadhili Solomon Muysa akiwa China Shanghai, Huko aliwakuta wanachama wa Chama cha Demokrasia na MAendeleo CHADEMA.

Wednesday, November 10, 2010

Fananisha taarifa hizi mbili!

Nikisema tumelogwa nitakuwa nakosea?? Hebu angalia hizi taarifa mbili. Ya kwanza inatoka kwenye chombo chenye dhamana ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini (TAKUKURU) na ya pili inatoka katika ubalozi wa Uingereza ambao ulihusishwa kwenye taarifa ya kwanza!!
**********************************************************************
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

YAH: UCHUNGUZI KUHUSU TUHUMA ZA RADA


Tunapenda kuujulisha umma kuwa uchunguzi na ushahidi uliokusanywa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) pamoja na Shirika la Upelelezi - SFO la Uingereza kuhusu tuhuma za Rushwa katika ununuzi wa Rada, umeshindwa kumhusisha Bw. Andrew Chenge katika tuhuma hizo.

TAKUKURU inawaomba wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa chombo hiki kwa kutoa taarifa za kuwafichua wale wote wanaojihusisha na Rushwa kwani jukumu hili ni la kila mmoja wetu.

Imetolewa na
Doreen J. Kapwani,
Afisa Uhusiano-TAKUKURU
Novemba 08 , 2010

S. L.P. 4865,
Dar Es Salaam.

Simu: 2150043-6/2150360 Nukushi: (022) 2150047 Barua pepe: dgeneral@pccb.go.tz Mtandao www.pccb.go.tz


**********************************************

PRESS RELEASE

10 November 2010

PCCB’S STATEMENT OF 8 NOVEMBER RELATING TO THE BAE/RADAR CASE
The British Government is aware of a statement made by the Prevention and Combating of Corruption Bureau (PCCB) on 8 November 2010. At this stage the case relating to BAe and its dealings in Tanzania is yet to go to court in the UK. It is therefore not possible to draw conclusions either way relating to those who were interviewed in connection with the case.

NOTES FOR EDITORS:

On 5 February 2010, the Serious Fraud Office (SFO) announced that it had reached a settlement with BAe following an investigation into a defence contract with the Government of Tanzania.

Regarding Tanzania, BAe has admitted that it failed to keep reasonably accurate accounting records in relation to its activities here. BAe has said it will plead guilty to the aforementioned offence, and that it will pay a sum of £30 million by way of a penalty and also for reparation to Tanzania. A hearing in the crown court will determine the amount of the financial order (fine) with the balance to be made available as an ex-gratia payment to the people of Tanzania.

The plea agreement between BAE and the SFO brought to an end all outstanding investigations by the SFO. However, because the plea agreement has not yet been before the crown court in the UK, it is not possible to say at this stage whether the agreement will stand.

A crown court judge will determine whether the plea agreement between the SFO and BAE can be accepted. The hearing will start on 23 November.
*******************************************************************************
Nionavyo mimi:
Taarifa hii peke yake inapaswa kuwawajibisha viongozi wa juu wa TAKUKURU ambao inaonekana wazi kabisa kwamba ni taasisi inayoendeshwa kwa kufuata matakwa ya watu wachache wenye uwezo zaidi! Hii ni aibu kubwa sana kwa taifa ambalo tumekuwa tukiimba kwamba tuna amani na haki! Ninatamani sana watoe tamko na ikiwezekana wajipe moyo na KUJIUZULU kwa manufaa ya taifa!!
Na mwisho kabisa naomba ninukuu Biblia takatifu ambayo inasema, "HAKI HUINUA TAIFA, BALI DHAMBI NI AIBU KWA WATU WOTE"
Dhambi ni pamoja na Rushwa, Uongo. Ninadhani kuna haja kubwa zaidi ya kuwa na siku moja ya kumuomba Mungu toba ya taifa maana watu wachache wamekuwa kama miungu watu na kutuharibia kiasi hiki!
Mungu ibariki Tanzania!

Blandina na Tusiime!

Hayawi hayawi hatimaye yamekuwa!!! Dada Blandina na kaka Tusiime hatimaye wafunga pingu za maisha na kuyaanza rasmi maisha ya ndoa siku ya jumamosi tarehe 6 Nov. Arusi yao ilifungwa katika kanisa la KKKT usharika wa mjini kati Arusha na kufuatiwa na sherehe ya ukweli katika ukumbi wa Triple A. Mapicha ndio haya!!

Tabasamu la matumaini kabla ya kuingia ukumbini!






Tusiime



Blandy.




Testing the muscles!!




Mambo ya keki!










Sasa hapa ni mambo ya ku dance kwa kwenda mbele!!



Kaka Gee akiserebuka na mama wa Blandina.




Kaka Gee na wife wakiwakilisha SBP ndani ya mjengo!
Familia nzima ya SBP inawatakia maisha mema sana ya ndoa marafiki zetu Tusiime na Blandina.

Monday, November 1, 2010

Jimbo la Arusha mjini sasa ni la CHADEMA!!

Hatimaye jimbo la Arusha mjini limechukuliwa na CHADEMA kutoka kwenye mikono ya CCM!! Mbunge mpya sasa atakuwa kaka Godbless Lema na amemuangusha aliyekuwa waziri wa serikali ya Kikwete Dr Batilda Burhani.

Na kwa mujibu wa TBC1 wameeleza kuwa ni habari ya kustusha sana kwa waziri wa kikwete kuanguka!!

Hongera sana Godbless Lema na hongera sana CHADEMA!!

Mungu ibariki Tanzania!

Katika picha hii ya mwaka jana mwishoni, Godbless Lema(kushoto) akiwa na kaka Gee!!

George na Emiliana wafunga pingu za Maisha

George and Emiliana
Pozi la Pamoja


George

Emiliana



Wapambe kibao



Pokea pete hii


Nathibitisha kua sisi ni Mume na Mke


Keki


Pozi la kutokea

Wapambe wa .dot com




Benz

Wazazi

Misosi

Maakuli



Muziki ulifunguliwa