Tafuta/Search This Blog

Friday, December 30, 2016

UZALENDO NI KUTEKELEZA WAJIBU WETU KWA MAMA TANZANIA - SEHEMU I

Kwa mara nyingine tunaendelea na mfululizo wa makala za kudadavua dhana ya uzalendo na wajibu wetu kwa nchi na yetu Tanzania, ambae kupitia maziwa tuliyonyonya na misingi aliyotujengea, leo hii tunaweza kujumuika na wanadunia wengine kupitia teknolojia ya habari na mawasiliano.
Leo, hii tuangalie dhana ya wajibu wetu kwa nchi yetu ni nini hususan, katika wakati huu wa mpito wa mageuzi ya kiuchumi na kiutawala mara baada ya kuingia madarakani mzawa wa chato na mbobezi wa kemia na hisabai Rais John Magufuli.
Viktor Frankl ni mtafiti wa wa tabia za wanadam kutafuta furaha (pursuit of happiness) na kupitia majarida kadha wa kadha ame-eleza kwa ufasaha ramani au michoro katika akili ya mwanadamu. Mtafiti huyu ameweka wazi namna akili inaweza kuendelezwa na kumfanya mtu kuwa na kitabia ya aina flani. Na tabia hiyo huwa ni mfumo wa maisha ya watu na hali kadhalika katika jamii husika.
Mathalani, jamii za Korea, Japan hata Malaysia mtu akishindwa kutimiza azma yake ya kutoa mchango kwa maendeleo ya jamii, huishia kujua. Wengi hujiua kwa kushindwa kukubaliana na uhalisia wa nje kama vile kufilisika, kuachishwa kazi ghafla hasa kama ulikuwa ni wadhifa mkubwa serikalini au kampuni za sekta binafsi. Tabia hii ilikuwa dhahiri sana nyakati za anguko la kiuchumi duniani ambalo pia liliathiri uchumi wa nchi hizo na makampuni yao kibiashara.
Kwa upande mwingine, mtafiti Frankil alikusudia kutufunulia na kutujuza matokeo ya kitabia ili kupata tija ya hali ya juu (highly effective) kutoka kwa mtu katika mazingira yoyote yale. Tija katika muktadha huu ni uwezo wa kuona na jicho la kutafuta jibu au suluhisho katika mazingira magumu au wakati tete katika jamii.
Kwa maana nyingine, “jicho la tatu” laweza kuitwa “proactivity”. Proactive kwa tafsiri rahisi ni hali ya kuwa na fikra ya kuanzisha jambo lenye kutatua tatizo linaloinzunguka jamii au nchi ya mhusika.
Dhana inayojengwa na inayotazamwa ni hali ya kumtaka mwanadamu kunawajibika na maisha yake kwa kuyakabili mazingira au changamoto za mazingira yanayomzunguka. Tukumbuke, tabia ya kila mwanadamu ni mwitikio wa maamuazi (behavior is a function of decision of an individual). Ni namga gani mtu anayakabili mazingira au hali inayomzunguka.
Tanzania inapitia katika changamoto ya kimtazamo na kifikra tokea Rais John Magufuli achukue hatamu ya kutuongoza. Rais Magufuli amekuja na mfumo wake wa kudhibiti matumizi ya serikali na kuziba mianya ya “kupiga dili” ndani ya serikali na katika sekta binafsi; ambayo ilikuwepo kupitia mambo kadha wa kadha kama wafanyakazi hewa, wanafunzi hewa ambao walipelekea malipo hewa kupigwa na wezi wachache.
Kufuatia kusudio lake la kusimika mfumo mpya, kuna namna baadhi ya shughuli za kibiashara zimeathirika kutegemea na misingi ya wenye biashara walivyokuwa wamejenga mifumo yao ya kuziendesha.
Tukichukua wajibu wetu ili kujipanga upya namna ya kuendana na mfumo mpya wa awamu ya tano, tunawajibika kuamua namna ya kufanya biashara kwa kuzingatia misingi halali ya kulipa kodi na kufuata sheria na msingi ya kufanya kibiashara ili kukidhi uhitaji wa soko au walaji.
Pengine, tupate maana ya neno wajibu. Wajibu lilitokana na neno la kingereza responsibility -- "response-ability" – nguvu ya mwitikio au uwezo na maamuzi ya kuchagua kutenda ikisukumwa na nguvu iliyo ndani ya mtu. Huo ndiyo wajibu au kuwajibika.
Hivyo basi, wajibu ni mwitikio na uwezo na kufanya maamuzi kuyatawala au kuyadhibiti mazingira, au kulia na kulalama dhidi ya hali iliyopo. Kama tunakumbuka, Rais Obama wakati ameingia madarakani mwaka 2009, Marekani na dunia ilikuwa na anguko kubwa la kiuchumi (global economic crisis). Obama na wenzie hawakulia na kumlaumu Bush na kukumbuka miaka nane ya Bill Clinton uchumi ulikuwa mzuri, walitimiza wajibu wao wa kujipanga na kujenga mfumo mpya na leo hii uchumi wa Marekani umeimarika tofauti na miaka 8 iliyopita.
Itaendelea…
Fredrick Matuja
fmatuja@hotmail.com

No comments: