Tafuta/Search This Blog

Wednesday, June 27, 2012

Kama ningekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania...

Haya ndio magari yangetumika na serikali na idara zake zote...

LANDROVER DEFENDER - watendaji wote wa idara za serikali zinazohitaji magari. Hii ni pamoja na wakuu wa  polisi magereza na jeshi.
SUZUKI JIMMY -  wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa mikoa na wilaya na wote katika TAMISEMI wanaohitaji magari kama wahandisi.

TOYOTA COROLLA - wakuu wa mikoa. Kama anataka kutoka nje ya mkoa atatumia Landrover Defender kama inayoonekana hapo juu. Gari kama hii pia itamfaa katibu mkuu kiongozi na watendaji wengine wa serikali.




TOYOTA RAV4 - mawaziri na manaibu waziri.
Najua mtalalamikia barabara zetu...badala ya kulalamika inatupasa tuzitengeneze maana kuna wanaolipa kodi kila siku na hawana hata baiskeli, hao huwa hawana pa kulalamikia.

No comments: