Tafuta/Search This Blog

Tuesday, July 31, 2012

Papaa On Tuesday......Ukitaka Kukubalika na Kila Mtu Utaboa.


Wakati Walimu Wakiwa Wanaingia Katika siku ya pili ya Mgomo Wao Usiokuwa na Kikomo siku ya Leo, Bungeni kunatarajiwa kulipuka kwa hoja ya kuhusiana na mgomo wa Madaktari sababu Wizara ya Afya na Ustawi Wa jamii iliwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi jana pamoja na mdahalo wa kuchangia siku ya leo.

Ninawasalimu Wasomaji Wangu wa ndani na nje ya nchi, nimefarijika sana baada ya kupokea simu za Waheshimiwa Wabunge Wanaofatilia Blog yangu hususan Papaa On Tuesday, siku si nyingi nitakuwa nanyi Mjengoni na kuandika Papaa On Tuesday nikiwa Bungeni, yote ni heri na Kila Jambo na Majira yake.

 Zangu salamu leo nazipeleka kwa wasomaji wangu walio kule hydom, maeneo ya Mbulu, Babati, Dongobesh na maeneo ya Jirani. Miaka michache iliyopita nakumbuka nilipita Kiteto nikaenda Mbulu, Kutoka Mbulu nilichukua landrover mpaka Dongobesh ambako nilifanya makazi yangu kwa Mchungaji wa KKKT Zakayo Malekwa. Ni safari yenye kukumbukwa sana. Siku chache zijazo nitakuwa huko Hydom kwa project mpya ya Blog nikishirikiana na Mwenyeji wangu Amani Paul Mzee Wa Kambi Popote.

Katika muda mchache nilioishi hapa duniani zaidi ya miaka 30 nimebaini huwezi kukubalika na kila mtu hata wale unaodhani ungetaka wakukubali katika kile unachokifanya. Kuna wakati nilikuwa na wakati mgumu sana kutaka kila mtu anielewe katika kila ninachofanya mwisho wa siku nilikua naumia hata baada ya kutaka kuwapendeza nikagundua bado kuna watu hawanikubali katika ninachokifanya.

Mara kadhaa nimefadhaika baada ya kuona hata lile ninalofanya kwa ajili ya Jamii kwa gharama zangu na muda wangu bado pia watu hawakukubali, mmoja wa marafiki zangu wa jinsia ya kike mara zote ninapokuwa niko disappointed huwa ananiambia maneno machache lakini yenye kunifikirisha kwanza huwa ananiambia "Think Positive and Take It Positive" na wakati mwingine huniambia "Nini sababu ya wewe kufanya, unataka kukubalika ama kutimiza kusudi?". Utakuwa unajisikia vibaya zaidi iwapo ulikuwa unataka kufanya ili ukubalike na kama kila kitu watu wanachosema unachukulia negative/hasi basi jua utavunjika moyo.
Mwana wa Mungu, Yesu Kristo hakukubalika na kila mtu sembuse wewe mtoto wa Filikunjombe?Duniani kuna watu wanamakwazo sana na kuna mtu mwingine yaani hakukubali hata kama haujafanya lolote. Maofisini kwetu ama hata makanisani na Jamii kwa ujumla kuna mtu inatokea tu hakukubali na pengine mpaka mtagombana, au anakukasirikia bila hata sababu na unaooteza muda kutafuta suluhu lakini haipatikani mwisho wa siku utasikia "damu yake na yangu haziendani".

Ukifanya mema duniani kuna watu watakukubali na kuna watu hawatakukubali wataona unatafuta tu sifa, ukifanya mabaya kuna watu watakukubali na kuna watu hawatakukubali, maana kila uovu una wafuasi wake. Ukitafuta kukubalika utaboa kwenye maisha yako.

 
Chochote ambacho unafanya kwa nia njema na una amani ya moyoni ambacho si uovu basi fahamu kuwa huwezi kukubalika na kila mtu. Mambo mangapi umefanya ambayo watu hawakukuelewa hata ulipowaelewesha lakini yamkini jambo hilo Mungu ameliruhusu kwenye maisha yako. Take it Positive kuna kujifunza katika kila shutumu ama lawama toka kwa watu wasiokukubali, yamkini wanachokiongea ukikitendea utakuwa bora zaidi. Katika kutimiza ndoto za maisha yako huwezi kupata wa kukupigia makofi kuna wakukuzomea pia na kukung`ong`a ili uweze kujitahidi. Biblia inasema jitahidi kwa bidii kuwa na amani na kila mtu suala la wao kukubali ama kuto kukubali ni uamuzi wao, usipoteze muda kumpendezesha mtu na kumkwaza Mungu, wanadamu wana yao. Ukitaka kila mtu akupigie makofi katika yale unayofanya basi jua kuna uwezekano mkubwa usitimize ndoto yako ukawa unatimiza ndoto za wengine.

Ukiwa mfugaji mkubwa watasema, ukiwa mfugaji mdogo watasema,ukiwa tajiri watasema, ukiwa masikini watasema, ukiwa mrefu watasema ukiwa mfupi watasema, Ukiwa mwembambaaaa watasema, Ukiwa Umejazia jazia Watasema, na hata usipokuwa chochote watasema.


Kila Mtu ameumbwa kwa namna ya tofauti, Kuna watu watakuchukia tu sababu unaweza kufanya wao hawawezi, Kuna watu watakuchukia sababu ya kazi yako, Kuna Watu watakuchukia sababu Cheo Chako anaona yeye ndiye anastahili, Kuna Watu Watakuchukia Sababu wewe huwa huchukii, Kuna watu leo hauna relationship ni ma best zako siku ukiwa na relationship utaona watu wanakuchukia, ukisema leo unaenda kuishi nje ya Tanzania kuna watu watakuchukia, Ukiamua leo Kuwa Mtakatifu kuna watu watakuchukia. Huwezi Kumpendeza Kila Mtu Utaboa

Mungu alituumba tofauti tofauti Kwa Sababu, Mungu akatupa utashi tofauti kwa Kila Mtu Kwa Sababu, Ukianza kuishi ili Kumpendeza fulani ama group fulani utaishia kupoteza Identity yako. Uliumbwa Kwa Sababu haukuumbwa kama boya, uko duniani kwa makusudi maalum wewe ni Project Manager wa Mungu duniani, Kuna Kitu Mungu anataka kufanya duniani kupitia wewe. Kulazimisha baadhi ya mambo kwenye maisha ni kupoteza kile ambacho Mungu anataka, Samaki hafundishwi kuogelea, Wala hakuna kisu kinachoenda Kujifunza Kukata, Kuna vitu vimo ndani yako hauhitaji Kujitahidi ili kuweza kufanya, huwa situmii Msuli Mkubwa Kuandika Papaa On Tuesday, Huwa Situmii Msuli kuongea, sababu ni Kama Samaki yuko baharini Kuogelea ni lazima, ninatambua kuna watu hawapendi vile nilivyo, Lakini Siishi Wao Watakavyo, Ila naishi nitakavyo.


Think Differently and Make a Difference.

No comments: