Tafuta/Search This Blog

Saturday, May 8, 2010

Jamani Moshi pasafi!!

Sina haja ya kuongea sana, lakini kwa kweli mjii huu nahisi una watendaji wanaofanya kazi. Pokeeni pongezi nyingi sana kutoka kwetu.
Lakini ajabu yake, kilometa 80 tu kutoka moshi kuna mji wa kitalii unaoitwa Arusha, kwa masikitiko kabisa mji huo ni mchafu. Hivi watu hawawezi hata kuiga tu au wanafikiria usafi ni mtihani kwamba wakiiga watafutiwa matokeo!! Inanikera sana!!

Hongera sana mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, na hongera sana viongozi wooote wa manispaa ya Moshi, pongezi nyingi pia kwa migambo woooote wa manispaa hii na tunawakaribisha sana Arusha!!

3 comments:

Subi Nukta said...

Yaa, hii picha ndiyo naiiba rasmi sasa, ukitaka kunishitaki nakubali, mi nimeipenda ngoja niipeperushe zaidi...

shalom broz productions said...

hahahahahaaaaaa, Subi mbabe!!! Haya bwana uwe na amani!

Subi Nukta said...

Asante.
Nimeshaikwapua, nimeshaipamba kule wavuti na nshakonga nyoyo za wakereketwa na nshapokea makala ya mtu aliandika kuhusu mji wa Moshi, naipanga vizuri tni niirushe hewani makala hiyo!
Ngoja nikakusanye mapicha meeeengi ya Moshi sasa...