Tafuta/Search This Blog

Sunday, October 27, 2013

Sikiliza kuhusu daktari aliyejitolea maisha kuokoa wahanga wa ubakaji!

Denis Mukwege, daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake kwa zaidi ya takribani miaka 15 amejitolea maisha yake kuokoa wahanga wa ubakaji huko mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC. Akihudumia kwenye hospitali ya Panzi huko Bukavu, hospitali aliyoianzisha mwaka 1993, Dkt. Mukwege na wenzake wametoa usaidizi wa kitabibu kwa maelfu ya wanawake waliokumbwa na wanaoendelea kukumbwa na madhila ya ubakaji. Katika makala hii, Joseph Msami alipata fursa kuzungumza na Dokta Mukwege ambaye alifika makao makuu ya Umoja wa Mataifa kwa mazungumzo na Katibu Mkuu Ban Ki-Moon. Katika mazunguzo na Msami, Dokta Mukwege walijadili mengi ikiwemo alivyonusurika kuuawa mwaka mmoja uliopita. 


No comments: